" DERBY YA WACHIMBAJI YAMALIZIKA, NYANDOLWA FC YAFUZU HATUA INAYOFUATA, BAJAJI FC YAAGA NIACHEKONA CUP 2026

DERBY YA WACHIMBAJI YAMALIZIKA, NYANDOLWA FC YAFUZU HATUA INAYOFUATA, BAJAJI FC YAAGA NIACHEKONA CUP 2026

Na Mapuli Kitina Misalaba

Baada ya ushindi wa mchezo wa kwanza, timu ya Nyandolwa FC imeendelea kuonesha ubabe wake katika mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Bajaji FC derby katika mchezo wa marudiano uliochezwa leo Juni 2, 2026 katika uwanja wa Mwabenda, Kata ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

Ushindi huo unaifanya Nyandolwa FC kufuzu hatua inayofuata ya mashindano hayo kwa jumla ya mabao 2-0, baada ya kushinda mchezo wa kwanza kwa bao 1-0 dhidi ya wapinzani wao Bajaji FC.

Kwa ushindi huo, Nyandolwa FC sasa itasubiri mshindi wa mchezo wa kesho ili kufahamu mpinzani wake katika hatua inayofuata ya NIACHEKONA CUP 2026.

Akizungumza baada ya mchezo huo, Katibu wa Mashindano hayo ametangaza kuwa mchezo unaofuata utachezwa kesho ambapo Lyabukande FC itamenyana na Shilabela FC katika pambano linalotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.

Ameendelea kuwakaribisha wananchi wa Solwa na maeneo jirani kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa Mwabenda ili kushuhudia vipaji vya vijana na burudani ya soka kupitia mashindano hayo.

Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na mdau wa michezo Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA kwa ufadhili wa shirika la Lushu Foundation ikiwa lengo ni kuibua vipaji vya vijana, kuimarisha amani na kuendeleza michezo katika jamii.

Kwa huduma za ushereheshaji wa shughuli mbalimbali, matangazo na matukio ya kijamii, MC NIACHEKONA anapatikana kupitia namba 0757 267 738.

"NIACHEKONA CUP MWABENDA – WEKA TU WEKE."





 

Post a Comment

Previous Post Next Post