
Na Mapuli Kitina Misalaba
Timu ya Isenengeja FC kutoka Mkoa wa Mwanza
imefanikiwa kutinga hatua ya timu 12 bora za mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026
baada ya kuibuka na ushindi wa mikwaju ya penati 3-1 dhidi ya Mwakitolyo No. 6
katika mchezo wa marudiano uliochezwa katika Uwanja wa Mwabenda, Kata ya Solwa,
Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.
Katika mchezo wa kwanza, Isenengeja FC iliibuka na
ushindi wa bao 1-0, huku mchezo wa leo Juni 5, 2026 ukiwashuhudia Mwakitolyo
No. 6 wakijibu mapigo kwa ushindi wa bao 1-0 ndani ya dakika 90 za kawaida.
Matokeo hayo yaliifanya jumla ya mabao katika michezo
yote miwili kuwa sare ya 1-1, hali iliyolazimu mshindi kupatikana kwa mikwaju
ya penati kwa mujibu wa kanuni za mashindano hayo.
Katika hatua hiyo ya maamuzi, Isenengeja FC walionesha
umakini mkubwa na kufanikiwa kushinda kwa penati 3-1, ushindi uliowapa tiketi
ya kusonga mbele huku safari ya Mwakitolyo No. 6 katika mashindano hayo
ikifikia tamati.
Baada ya mchezo huo, viongozi wa Mwakitolyo No. 6
walimshukuru mwandaaji wa mashindano hayo kwa kuwapa nafasi ya kushiriki
NIACHEKONA CUP 2026, huku wakitoa pole kwa mashabiki wao waliokuwa na matumaini
ya kuwaona wakifika hatua za mwisho za mashindano hayo.
Kwa upande wa Isenengeja FC, ushindi huo unaifanya
timu hiyo kukutana na Kimandaguli FC katika hatua inayofuata ya mashindano
hayo, baada ya Kimandaguli FC kufuzu jana kwa ushindi wa penati dhidi ya
Kashishi FC.
Akizungumza baada ya mchezo huo, Katibu wa Kamati ya
Mashindano, Sambayi Jilya, ametangaza kuwa mchezo wa kesho utawakutanisha Bulige
FC kutoka Wilaya ya Kahama na Sangu FC kutoka Mkoa wa Mwanza katika pambano
linalotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.
Ameendelea kuwakaribisha wananchi, wadau wa michezo na
mashabiki wa soka kujitokeza kwa wingi katika Uwanja wa Mwabenda ili kuendelea
kushuhudia vipaji vya vijana na burudani ya michezo inayotolewa kupitia
mashindano hayo.
Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na mdau
wa michezo Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA kwa ufadhili wa shirika la
Lushu Foundation, yakiwa na lengo la kuibua vipaji vya vijana, kuimarisha amani
na kukuza michezo katika jamii.
Kwa mawasiliano ya huduma za ushereheshaji wa shughuli
mbalimbali, matangazo na matukio ya kijamii, MC NIACHEKONA anapatikana kupitia
namba 0757 267 738.
Kikosi cha Isenengeja FC.
Wachezaji wa Isenengeja FC na Mwakitolyo No. 6 wakioneshana ushindani mkubwa katika mchezo wa marudiano wa NIACHEKONA CUP 2026.
Wachezaji wa Isenengeja FC na Mwakitolyo No. 6 wakioneshana ushindani mkubwa katika mchezo wa marudiano wa NIACHEKONA CUP 2026.
Viongozi wa mashindano wakifuatilia kwa makini pambano kati ya Isenengeja FC na Mwakitolyo No. 6 katika Uwanja wa Mwabenda.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
























Post a Comment