" NIACHEKONA CUP YAPAMBA MOTO, SANGU FC KUSHUKA DIMBANI LEO KUTETEA UBINGWA WAKE

NIACHEKONA CUP YAPAMBA MOTO, SANGU FC KUSHUKA DIMBANI LEO KUTETEA UBINGWA WAKE



Na Mapuli Kitina Misalaba

Macho na masikio ya mashabiki wa soka leo yataelekezwa katika Uwanja wa Mwabenda, Kata ya Solwa, ambapo mabingwa watetezi wa NIACHEKONA CUP, Sangu FC kutoka Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza, watashuka dimbani kumenyana na Bulige FC kutoka Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga katika mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.

Sangu FC wanaingia katika mchezo huo wakiwa na dhamira ya kuendelea kutetea ubingwa wao walioutwaa katika msimu wa 2024/2025, huku Bulige FC nao wakisaka ushindi utakaowaweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele kwenye mashindano hayo.

Pambano hilo linafunga rasmi hatua ya kwanza ya mzunguko wa pili wa mtoano wa NIACHEKONA CUP 2026, hatua iliyoshuhudia timu mbalimbali zikipambana kusaka nafasi ya kuingia katika kundi la timu 12 bora za mashindano hayo.

Mashabiki wengi wamekuwa wakijiuliza kama Sangu FC wataendelea kuonyesha makali yao na kuthibitisha ubora wao kama mabingwa watetezi au kama Bulige FC wataweza kuandika historia kwa kuwazuia kuendelea na safari ya kutetea ubingwa.

Baada ya mchezo wa leo, kuanzia Jumapili Juni 7, 2026, mashindano yataingia rasmi katika hatua ya timu 12 bora, ambapo mfumo wa mashindano utakuwa wa mtoano wa moja kwa moja (Knockout).

Katika hatua hiyo, timu zitakapokutana mshindi ataendelea na mashindano huku timu itakayofungwa ikiondolewa moja kwa moja, hali inayotarajiwa kuongeza ushindani na presha kwa kila timu.

Baadhi ya michezo iliyopangwa kuchezwa katika hatua ya timu 12 bora ni pamoja na:

Nyundo FC dhidi ya Mawemiru FC, Duara FC dhidi ya Songambele Mhangu FC na Home Boys FC dhidi ya Ufukunyungu FC

Mashabiki wa soka na wadau wa michezo wameendelea kuhamasishwa kujitokeza kwa wingi katika Uwanja wa Mwabenda ili kushuhudia vipaji vya vijana vinavyoendelea kuibuliwa kupitia mashindano hayo.

Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na mdau wa michezo Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA kwa ufadhili wa shirika la Lushu Foundation, yakiwa na lengo la kuibua vipaji vya vijana, kuimarisha amani na kukuza michezo katika jamii.

Kwa mawasiliano ya huduma za ushereheshaji wa shughuli mbalimbali, matangazo na matukio ya kijamii, MC NIACHEKONA anapatikana kupitia namba 0757 267 738.

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

 

Post a Comment

Previous Post Next Post