" WATU 75 AWASHIKILIA KWA TUHUMA ZA VURUGU SHINYANGA

WATU 75 AWASHIKILIA KWA TUHUMA ZA VURUGU SHINYANGA


Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga linawashikilia watu 75 kwa tuhuma za kufanya vurugu, kuwajeruhi watumishi wa umma pamoja na kushiriki vitendo mbalimbali vya uhalifu katika Kijiji cha Sanjo, Kata ya Idukilo, Wilaya ya Kishapu.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Janeth Magomi, amesema matukio hayo yalitokea kati ya Mei 28 na Juni 1, 2026 wakati watumishi wa umma walipokuwa wakitekeleza majukumu yao katika eneo hilo.

Amesema watuhumiwa hao wanadaiwa kushiriki katika vitendo vya uvunjifu wa amani vilivyosababisha baadhi ya watumishi wa umma kujeruhiwa pamoja na kuathiri utekelezaji wa shughuli mbalimbali za serikali katika eneo husika.

Kamanda Magomi amesema Jeshi la Polisi lilifanya operesheni maalum kufuatia matukio hayo na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao ambao kwa sasa wanaendelea kuhojiwa huku uchunguzi ukiendelea kubaini ushiriki wa kila mmoja wao.

Amesisitiza kuwa Jeshi la Polisi halitavumilia vitendo vya uvunjifu wa sheria na kwamba hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya yeyote atakayebainika kuhusika na matukio hayo.

Aidha, amewataka wananchi kuendelea kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama kwa kutoa taarifa za wahalifu na kuepuka kushiriki katika vitendo vinavyoweza kuhatarisha amani na usalama wa wananchi.

Kamanda Magomi amebainisha kuwa baada ya kukamilika kwa uchunguzi, watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili kwa mujibu wa sheria.

 SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post