Na Mapuli Kitina Misalaba
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Julius Mtatiro, amewataka
wazazi na walezi kuacha tabia ya kuwakatisha tamaa watoto wa kike katika safari
yao ya elimu, akisisitiza kuwa serikali haitavumilia mtu yeyote anayekiuka haki
ya mtoto kupata elimu.
Mtatiro ametoa kauli hiyo, wakati wa Tamasha la
Kitaaluma 2026 ambalo limefanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Old Shinyanga, ambapo walimu na
wanafunzi kutoka shule mbalimbali wameshiriki mashindano ya michezo pamoja na
utoaji wa tuzo kwa waliofanya vizuri kitaaluma.
Akizungumza katika tamasha hilo, Mtatiro amesema
anaendelea kupigania elimu ya mtoto wa kike kwa sababu anaamini ndiyo msingi wa
kupata viongozi bora wa baadaye.
Amesema serikali itaendelea kuchukua hatua kali dhidi
ya wazazi au walezi watakaobainika kuwazuia watoto, hususan wa kike, kuendelea
na masomo kwa sababu elimu ndiyo njia ya kuwawezesha kujitegemea na kuchangia
maendeleo ya taifa.
Mbali na hilo, Mtatiro aliahidi kuanzisha tamasha la
michezo na taaluma kwa walimu pamoja na wanafunzi, na kwamba ahadi hiyo sasa
imetekelezwa kwa mafanikio makubwa ambapo amesema ataendelea kuanda matamasha ya
michezo kwa ajili ya wanafunzi.
Ameeleza kuwa tamasha hilo limeongeza mshikamano kati
ya walimu na wanafunzi, limeimarisha afya kupitia michezo na limewapa nafasi ya
kubadilishana uzoefu unaochochea matokeo bora ya kitaaluma.
Kwa upande wake, Kaimu Afisa Elimu wa Shule za
Sekondari Manispaa ya Shinyanga, Richard Makoye, amesema tamasha hilo limekuwa
sehemu muhimu ya kuunganisha walimu na wanafunzi, kujenga afya, ushirikiano na
kuongeza ari ya kujifunza na kufundisha.
Makoye amesema mafanikio hayo yanatokana na mazingira
mazuri yanayoendelea kuwekwa na Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan
katika kuimarisha sekta ya elimu nchini, huku akiipongeza Ofisi ya Mkuu wa
Wilaya kwa kuendeleza utaratibu huo unaochangia maendeleo ya elimu.
Naye Mkuu wa Shule ya Sekondari Ndala, Hamisa Magulu,
amesema tamasha hilo limekuwa na manufaa makubwa kwa kuwa limeimarisha
mahusiano kati ya shule mbalimbali na kusaidia kupunguza changamoto za afya ya
akili kupitia ushiriki wa michezo.
Mmoja wa wanafunzi, Daud Charles wa Shule ya Sekondari
Old Shinyanga, amesema michezo hiyo imewajengea afya njema, ushirikiano na
kuwatia moyo wa kufanya vizuri zaidi katika masomo.
Katika tamasha hilo kumefanyika mashindano mbalimbali
ikiwemo mpira wa miguu, mpira wa pete, mpira wa kikapu, mpira wa wavu, riadha,
kufukuza kuku, kukimbia na magunia, draft, bao, karata pamoja na michezo
mingine ya burudani.
Washindi wa mashindano mbalimbali wamekabidhiwa zawadi, huku walimu na shule zilizofanya vizuri kitaaluma zikitunukiwa vyeti vya pongezi. Katika fainali ya mpira wa miguu, timu ya wanafunzi wa Kidato cha Sita wa Shule ya Sekondari Old Shinyanga iliibuka bingwa baada ya kuifunga timu ya Kidato cha Nne mabao 2-0, na kukabidhiwa kombe, mbuzi watatu pamoja na vinywaji.
Mchezo wa kukimbia kwenye Magunia ukiendelea.
Picha ya pamoja kuelekea mechi ya kidato cha sita na kidato cha nne kwa wanafunzi wa shule ya Old Shinyanga.
DC Mtatiro akiendelea na zoezi la kukabidhi vyeti kwa shule na walimu waliofanya vizuri kwenye masomo yao katika mitihani ya taifa 2025.
DC Mtatiro akiendelea na zoezi la kukabidhi vyeti kwa shule na walimu waliofanya vizuri kwenye masomo yao katika mitihani ya taifa 2025.
DC Mtatiro akiendelea na zoezi la kukabidhi vyeti kwa shule na walimu waliofanya vizuri kwenye masomo yao katika mitihani ya taifa 2025.
DC Mtatiro akiendelea na zoezi la kukabidhi vyeti kwa shule na walimu waliofanya vizuri kwenye masomo yao katika mitihani ya taifa 2025.
DC Mtatiro akiendelea na zoezi la kukabidhi vyeti kwa shule na walimu waliofanya vizuri kwenye masomo yao katika mitihani ya taifa 2025.
DC Mtatiro akiendelea na zoezi la kukabidhi zawadi kwa washindi wa michezo mbalimbali katika tamasha hilo.
DC Mtatiro akiendelea na zoezi la kukabidhi zawadi kwa washindi wa michezo mbalimbali katika tamasha hilo.
DC Mtatiro akiendelea na zoezi la kukabidhi zawadi kwa washindi wa michezo mbalimbali katika tamasha hilo.SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254








































































































Post a Comment