
Jukwaa la Viongozi Wanawake nchini (WLF) limesema amani, umoja na maridhiano ya kisiasa ni msingi wa maendeleo ya taifa, likiwataka Watanzania kuweka maslahi ya nchi mbele kuliko tofauti za kisiasa.
Makamu Mwenyekiti wa WLF, Azza Haji Suleiman, amesema usalama wa Zanzibar una mchango mkubwa katika kuimarisha usalama wa Muungano, akisisitiza umuhimu wa mshikamano wa wananchi.
WLF imesema utulivu wa kisiasa huwezesha uwekezaji, ajira na ukuaji wa uchumi, huku ikitaka ushindani wa kisiasa ubaki kwenye sanduku la kura na vyama kushirikiana katika masuala ya maendeleo.
Jukwaa hilo limepongeza hatua ya viongozi wa CCM na ACT-Wazalendo kusaini Tamko la Pamoja la Mwafaka wa Kisiasa Zanzibar, likisema kulinda amani ni jukumu la kila Mtanzania.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
Post a Comment