" MIRADI YA SH.BILIONI 101.9 KUPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWANZA

MIRADI YA SH.BILIONI 101.9 KUPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWANZA



Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda amesema Mkoa huo umekamilisha maandalizi ya mapokezi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026 zitakazoingia mkoani humo Agosti 10 kupitia Wilaya ya Ukerewe na kuondoka Agosti 18 kuelekea Mkoa wa Shinyanga.

Amesema Mwenge huo utatembea kilometa 941 katika halmashauri zote nane za Mkoa wa Mwanza, ukipitia miradi 51 ya maendeleo yenye thamani ya Shilingi bilioni 101.9.

Kwa mujibu wa RC Mtanda, miradi hiyo inahusisha sekta za maji, afya, elimu, barabara, mazingira na nishati safi, ambapo baadhi itazinduliwa, kuwekwa mawe ya msingi, kufunguliwa na kukaguliwa.  


Amewataka wananchi wa Mwanza kujitokeza kushiriki shughuli za Mwenge wa Uhuru, akisema ni fursa ya kuonesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuimarisha 

Post a Comment

Previous Post Next Post