" CHIFU SANGALALI AWATAKA WANAFUNZI WA KIKE KUSOMA KWA BIDII, AWAONYA KUTOA KIPAUMBELE NDOA

CHIFU SANGALALI AWATAKA WANAFUNZI WA KIKE KUSOMA KWA BIDII, AWAONYA KUTOA KIPAUMBELE NDOA

Mwenyekiti wa Machifu Tanzania na Mtemi wa Himaya ya Jigoku, Chifu Antonia Sangalali, amewataka wanafunzi, hususan wa kike, kusoma kwa bidii na kuweka elimu mbele ili waweze kutimiza ndoto zao na kujenga maisha yao ya baadaye.

Chifu Sangalali ametoa ujumbe huo wakati wa Tamasha la 19 la Himaya ya Jigoku, Masela, Wilaya ya Maswa mkoani Simiyu, akiwataka wanafunzi kutokukimbilia kuolewa na kuacha masomo.

Amesema elimu ni msingi muhimu wa maisha na amewataka wanafunzi kutumia fursa wanazopata shuleni kwa kujituma katika masomo badala ya kuacha elimu kwa sababu ya kuingia kwenye ndoa wakiwa bado katika hatua ya masomo.

“Nitumie fursa hii kuwahimiza wanafunzi, hasa wa kike, someni sana, msikimbilie kuolewa mkaacha masomo,” amesema Chifu Sangalali.

Amesema jamii ina wajibu wa kuwaunga mkono watoto katika safari yao ya elimu na kuhakikisha wanapata mazingira yanayowawezesha kusoma na kutimiza malengo yao.

Ujumbe huo umetolewa katika tamasha hilo lililolenga pia kuendeleza mila na tamaduni za Kitanzania, kuimarisha mshikamano na kutoa elimu mbalimbali kwa jamii.

Chifu Sangalali amesisitiza kuwa vijana wenye elimu wana nafasi kubwa ya kuchangia maendeleo ya familia zao, jamii na taifa, hivyo amewataka wanafunzi kutumia muda wao vizuri na kuweka juhudi katika masomo yao.

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post