Ujumbe wa
amani, mshikamano na kuheshimu mila na tamaduni za Kitanzania umetawala katika
Tamasha la 19 la Himaya ya Jigoku, Masela, Wilaya ya Maswa mkoani Simiyu,
lililoandaliwa na Mwenyekiti wa Machifu Tanzania na Mtemi wa Himaya hiyo, Chifu
Antonia Sangalali.
Akizungumza
katika tamasha hilo, Chifu Sangalali amewataka wananchi kuendelea kuitunza
amani ya Tanzania, kuheshimu Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na
kuzingatia maadili katika maisha ya kila siku.
Amesema
matamasha hayo yanayofanyika kila mwaka yakiwa na burudani za ngoma za asili ni
sehemu ya kuwaunganisha wananchi, kuendeleza mila na tamaduni pamoja na kutoa
elimu mbalimbali kwa jamii.
Chifu
Sangalali amesema amani ni msingi wa maendeleo na ustawi wa jamii, hivyo
wananchi wanapaswa kuilinda na kuepuka vitendo vinavyoweza kuvuruga utulivu wa
nchi.
“Tuendelee
kuiheshimu Serikali yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tuendelee kuiweka
amani mbele na maadili tuyafuate ili tuweze kuishi kwa amani,” amesema Chifu Sangalali.
Kwa upande
wake, mgeni rasmi katika tamasha hilo, Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dkt. Vicent
Anney, amempongeza Chifu Antonia Sangalali kwa kuendelea kuandaa tamasha hilo
kila mwaka, akisema limekuwa sehemu muhimu ya kuhifadhi historia, mila na
tamaduni za Tanzania.
Amewataka
wananchi, hususan vijana, kuendelea kudumisha amani, mshikamano na kuheshimu
mila na desturi za Kitanzania.
“Bila
utamaduni wetu kuuheshimu taifa litapotea. Ili tuwe na taifa bora lazima
tutunze mila na desturi zetu. Niwaombe hasa vijana tutunze amani na
mshikamano,” amesema
Dkt. Anney.
Baadhi ya
wakazi wa Himaya ya Jigoku wamepongeza juhudi za Chifu Sangalali za kuendelea
kuandaa tamasha hilo kila mwaka, wakisema limekuwa likiwakutanisha ndugu na
jamii kwa ujumla, huku likitoa nafasi ya kubadilishana ujumbe wa amani, maadili
na umuhimu wa kutunza mila na tamaduni.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254




Post a Comment