" ASKOFU SANGU AFANYA UTEUZI KWA MAPADRE WAWILI JIMBO LA SHINYANGA

ASKOFU SANGU AFANYA UTEUZI KWA MAPADRE WAWILI JIMBO LA SHINYANGA

 Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu, amefanya mabadiliko madogo ya vituo vya kazi kwa Mapadre wawili wa Jimbo.

Askofu Sangu amefanya mabadiliko hayo Jumapili tarehe 16.04.2023, katika Misa ya maadhimisho ya kilele cha hija ya Huruma ya Mungu, ambayo imefanyika katika Kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Nkololo wilayani Bariadi mkoani Simiyu.
Katika mabadiliko hayo, Askofu Sangu amemteua aliyekuwa Paroko msaidizi wa Parokia ya Ng'wanhuzi Padre Peter Kija kuwa Paroko mpya wa Parokia teule ya Langangabilili, ambapo aliyekuwa Paroko wa Parokia hiyo Padre Pius Masubi, amemteua kuwa Paroko msaidizi wa Parokia ya Chamugasa.

Post a Comment

Previous Post Next Post