
Wakristo wamewatakiwa
kuacha uvivu kwa kudanganyika kwamba, wanaweza kupata mafanikio na utajiri kwa
njia ya kuwakimbilia viongozi wa dini ili wawapatie miujiza, na badala yake
wanapaswa kuomba huku wakifanya kazi kwa bidii.
Akitoa mafundisho ya
kiimani kupitia Misa ya Dominika ya Matawi, Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la
Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu ameonya kuwa, pamoja na kwamba Mungu anao
uwezo wa kumpa binadamu mafanikio, lakini mafanikio hayo hayaji kwa watu kukaa
na kusubiri miujiza badala ya kufanya kazi.
Askofu Sangu amewataka
Wakristo wote kuwa na imani thabiti isiyojaribiwa, huku akiwatahadharisha
kujiepusha na wimbi la watu wanotumia neno la Mungu kuwalaghai na kuwaaminisha
kuwa, wanaweza kuwapa mafanikio na utajiri ikiwemo nyumba na magari kwa njia ya
miujiza bila ya kufanya kazi, ambapo wakati mwingine hutumia fursa hiyo
kuwafanyia matendo yanayodhalilisha utu wao.
Katika hatua nyingine,
Askofu Sangu amewakumbusha watu wenye nafasi mbalimbali katika utumishi wa umma
na huduma za jamii kuzingatia misingi ya haki, ikiwa ni pamoja na kuepuka
kumkosea Mwenyezi Mungu kwa kutumia nafasi walizonazo kama fursa ya
kujinufaisha kupitia shida za wengine.
Ametumia nafasi hiyo
kuwasihi watalaam wa afya kuwahudumia wagonjwa kwa upendo na uaminifu, kwani
kwa kufanya hivyo watajiweka karibu zaidi na mwenyezi Mungu.
Askofu Sangu amewakumbusha Wakristo wote kudhihirisha imani yao ndani ya jamii kwa kudhibiti roho ya wivu na kufurahia mafanikio ya wengine pamoja na kuwa chimbuko la faraja, utulivu, matumaini na amani ndani ya jamii.
Askofu wa Kanisa
Katoliki Jimbo la Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu akitoa mafundisho ya
kiimani kupitia Misa ya Dominika ya Matawi

Misa ya Dominika ya Matawi ikiendelea katika
Kanisa kuu la Mama mwenye Huruma Ngokolo mjini Shinyanga

Misa ya Dominika ya Matawi ikiendelea katika
Kanisa kuu la Mama mwenye Huruma Ngokolo mjini Shinyanga

Misa ya Dominika ya Matawi ikiendelea katika
Kanisa kuu la Mama mwenye Huruma Ngokolo mjini Shinyanga

Misa ya Dominika ya Matawi ikiendelea katika
Kanisa kuu la Mama mwenye Huruma Ngokolo mjini Shinyanga

Misa ya Dominika ya Matawi ikiendelea katika
Kanisa kuu la Mama mwenye Huruma Ngokolo mjini Shinyanga

Misa ya Dominika ya Matawi ikiendelea katika
Kanisa kuu la Mama mwenye Huruma Ngokolo mjini Shinyanga
Post a Comment