Na Elisha Petro, Misalaba
Blog
Mkuu wa wilaya ya Maswa Mkoani
Simiyu Aswege Kaminyonge amewakumbusha
wazazi na walezi kuwajibikia vyema jukumu la malezi na makuzi bora ili kujenga
jamii na taifa lenye maadili mema.
Ameyasema hayo kwenye
hafla fupi ya kukabidhi baiskel zenye magurudumu matatu kwa watoto wawili wenye
ulemavu wa viungo zilizotolewa na shirika la Cathoric Relief Service (CRS) ililiyofanyika
katika shule ya Msingi Malampaka.
DC Kaminyonge amesema ni
wajibu wa wazazi na walezi kuhakikisha wanawalinda watoto dhidi ya mazingira
hatarishi hali ambayo itasaidia kuwa na taifa lenye kizazi chenye uadilifu.
Amewataka watoto hao,
wazazi pamoja na walezi kuhakikisha wanatunza baiskel hizo ili ziweze kudumu.
Wakati huo huo
amekumbusha wazazi na walezi kuwajibikia jukumu la kuchangia chakula shuleni
kama njia sahihi ya kuweka mazingira wezeshi ya ufaulu wa wanafunzi.
Kwa upande wake Paroko wa
Parokia ya Malampaka katika kanisa katoliki la Mama wa huruma Padre Renatus Mashenene ameshukuru na kupongeza
juhudi za Askofu wa jimbo katoliki la shinyanga mhasham Liberatus Sangu kuliruhusu
Shirika la Cartas kuendelea kushirikiana na jamii katika kutatua changamoto
mbalimbali.
Mkuu wa wilaya ya Maswa Mkoani
Simiyu Aswege Kaminyonge akiwa ameshikilia Baskel ya magurudumu matatu
Mkuu wa wilaya ya Maswa Mkoani
Simiyu Aswege Kaminyonge akikabidhi baskel kwa mtoto wenye ulemavu wa viungo
huku akiwa ameambatana na mama yake mzazi
Mkuu wa wilaya ya Maswa Mkoani
Simiyu Aswege Kaminyonge akikabidhi baskel kwa mtoto wenye ulemavu wa viungo
huku akiwa ameambatana na mama yake mzazi
Zoezi la Mkuu wa wilaya
ya Maswa Mkoani Simiyu Aswege Kaminyonge kukabidhi baskel kwa watoto wenye
ulemavu wa viungo likiendelea katika viwanja vya shule ya msingi Malampaka
Zoezi la Mkuu wa wilaya
ya Maswa Mkoani Simiyu Aswege Kaminyonge kukabidhi baskel kwa watoto wenye
ulemavu wa viungo likiendelea katika viwanja vya shule ya msingi Malampaka
Post a Comment