" SHIRIKA LA NANCY FOUNDATION NA UBONGO LEARING WAANZA KUTEKELEZA MRADI, WAIBUA WATOTO WA MITAANI 45 MJINI SHINYANGA

SHIRIKA LA NANCY FOUNDATION NA UBONGO LEARING WAANZA KUTEKELEZA MRADI, WAIBUA WATOTO WA MITAANI 45 MJINI SHINYANGA

Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Mashirika mawili yasiyokuwa ya kiserikali Mkoani Shinyanga Nancy Foundation na Ubongo learing yameanza kutekeleza mradi wa kupunguza watoto wa mtaani unaoitwa  “Home is where the heart is”.

Akizungumza kwenye hafla maalum ya kutambulisha mradi huo Mkurugenzi na mratibu wa shirika la Nancy Foundation katika programu ya marafiki wa watoto Bwana Ezra Manjerenga, amesema hatua hiyo itasaidia kupunguza na badaye kutokomza kabisa watoto wa mtaani.

Amesema mradi huo utatekelezwa kwa kipindi cha Miezi mitatu na kwamba utakuwa endelevu ukifanyika kwa kushirikiana na serikali pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Askari wa jeshi la akiba mgambo Ezekia Isaka ambaye ameshirikiana na mashirika hayo kuwafikia watoto wanaoishi mitaani ameeleza hali halisi ilivyo

“Tulikuwa tunawakuta kwenye changamoto ya Stendi ya mabasi wanaomba omba wanakula vyakula ambavyo havieleweki tulienda pia mtaa wa Ibinzamata tulifanikiwa kupata watoto watano tukaja kupata tena watoto wengine maeneo ya relini watoto wengine tumekuja kuwapatia hapa kata ya mjini”.amesema Mgambo Ezekia Isaka

Misalaba Blog imezungumza na baadhi ya watoto ambapo wametaja kuwa changamoto ya wazazi kutowapatia mahitaji ya muhimu ikiwemo chakula na vifaa vya shule ndiyo chanzo ambacho kinapelekea kukimbilia mitaani ikiwa lengo lao ni kwenda kuomba msaada hasa chakula.

Baadhi ya maafisa watendaji wa serikali walioshiriki katika zoezi hilo akiwemo Afisa ustawi wa jamii Manispaa ya Shinyanga Ancila Katero, Afisa maendeleo ya jamii kata ya Mjini Shinyanga Blandina Joseph Mwinamila pamoja na mtoa elimu kutoka Polisi dawati la jinsia na watoto wametoa wito kwa wazazi na walezi kusimamia vyema makuzi ya watoto ili kudhibiti ongezeko la watoto wa mitaani.

Jumla ya watoto 45 waliokuwa wakiishi katika mazingira hatarishi kwenye mitaa mbalimbali ya Manispaa ya Shinyanga wamekusanywa na kupatiwa elimu ya malezi na maadili April 14,2023


Baadhi ya watoto wakipata chakula cha pamoja na mratibu wa shirika la Nancy Foundation katika programu ya marafiki wa watoto Bwana Ezra Manjerenga

Mkurugenzi na mratibu wa shirika la Nancy Foundation katika programu ya marafiki wa watoto Bwana Ezra Manjerenga akizungumza baada ya zoezi hilo kutamatika

Afisa maendeleo ya jamii kata ya Mjini Shinyanga Blandina Joseph Mwinamila akizungumza na Misalaba Blog baada ya zoezi hilo kutamatika 

Post a Comment

Previous Post Next Post