" SERIKALI, SHIRIKA LA NANCY FOUNDATION NA UBONGO LEARING WAREJESHA WATOTO KWENYE FAMILIA ZAO SHINYANGA.

SERIKALI, SHIRIKA LA NANCY FOUNDATION NA UBONGO LEARING WAREJESHA WATOTO KWENYE FAMILIA ZAO SHINYANGA.

Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Serikali imesema kuwa ili kuondoa changamoto ya watoto kuishi katika mazingira hatarishi mitaani, ipo haja kwa wazazi na walezi kuwajibikia vema jukumu la malezi na makuzi bora.

Kauli hiyo imetolewa na Afisa ustawi wa jamii wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Bi. Ansila Materu baada ya kukamilika kwa zoezi la kuwakabidhi katika familia zao watoto wanne waliokuwa wakiishi mitaani shughuli ambayo ilifanyika kwa kushirikiana na mashirika mawili yasiyokuwa ya kiserikali Mkoani Shinyanga Nancy Foundation na Ubongo learing.

Afisa ustawi wa jamii huyo Bi. Ansila Katero ametaja baadhi ya sababu zinazochangia  watoto kutoroka nyumbani kwa wazazi au walezi wao kuwa ni pamoja na  kukosa mahitaji muhimu ikiwemo chakula.

Amesema zoezi la kuwarejesha watoto kwenye familia zao litakuwa endelevu katika Manispaa ya Shinyanga.

“Tunashukuru zoezi letu na kutambua watoto wanaozurula mitaani lipo katika hatua nzuri ni siku ya pili tumefanya zoezi hili kwa siku ya kwanza tulipata watoto kumi na nane (18 ) leo tumefanikiwa kuongeza watoto sita (6)  na watoto wanne (4) tumebahatika kuzungumza na wazazi wao  na kuwasihi ili tuweze kupata suluhisho la kuwasaidia watoto hawa”.

“Ila tulichogundua katika zoezi hili kinachosababisha asilimia kubwa watoto kutoroka nyumbani ni ile hali ya wazazi kuwa bize na shughuli zao kwahiyo hawana muda wa kukaa na watoto”

“Kwahiyo tunawasihi wazazi wawe karibu na watoto wawafuatilie watoto mashuleni pia wanapotoka nyumbani wahakikishe wanaacha chakula kwa ajili ya watoto kwa sababu changamoto wanasema wanaenda mitaani kwa ajili ya kutafuta chakula lakini pia wazazi tuwapangia watoto kazi za kufanya ili wasiende kuzurula”.amesema Afisa ustawi Ansila

Baadhi ya wazazi na walezi waliokabidhiwa watoto wao waliokuwa wakiishi mtaani wameshukuru na kupongeza juhudi za serikali kwa kushirikiana na mashirika hayo mawili Nancy Foundation na Ubongo learing kutekeleza mradi huo unaolenga kuwaondoa watoto wanaokimbilia mitaani.

Mashirika hayo mawili Nancy Foundation na Ubongo learing yanatekeleza mradi wa Miezi mitatu unaolenga kupunguza au kumaliza kabisa watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani katika Manispaa ya Shinyanga.

Shirika la  Nancy Foundation na Ubongo learing kwa kushirikiana na serikali ( Maafisa ustawi wa jamii Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga) wakiwa kwenye mazungumzo ya pamoja na mzazi wa mtoto katika kata ya Kitangili Manispaa ya Shinyanga.

Afisa ustawi wa jamii wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Bi. Lemiflora Nyalaja akizungumza ni mmoja wa watoto waliorejeshwa nyumbani kwa wazazi wao katika Manispaa ya Shinyanga.


Post a Comment

Previous Post Next Post