" WALINDA AMANI WA SAMIDRC WAANZA KUONDOKA CONGO.

WALINDA AMANI WA SAMIDRC WAANZA KUONDOKA CONGO.


Na Belnardo Costantine, Misalaba Media 

Walinda amani wa "SAMIDRC" waliotumwa chini ya Mwamvuli wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC)  waliokua wakilinda amani nchini  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, wameanza kuondoka, kupitia Rwanda mnamo Aprili kulindi nchini kwao.


Kikosi cha SADC, kinachojumuisha Wanajeshi kutoka Afrika Kusini, Tanzania na Malawi, kilifanya mchakato wa awali kwa uhakiki rasmi hati katika kivuko kikuu cha mpaka kati ya Rwanda na DRC kisha kuanza zoezi la kuondoka  nchin DRC leo tarehe 29/4/2024 wao pamoja na vifaa vyao vya kijeshi.

Hatahivyo idadi kamili ya Wanajeshi waliohusika na zoezi hilo  haijawekwa wazi kutokana na ombi la SADC.
Taarifa zinasema kundi  hili la awali kuondoka  ililenga kurudisha vifaa vya kijeshi sambamba na kikosi kidogo cha askari, huku makundi makubwa yakitarajiwa kufuata.
Wanajeshi hao wanasafiri kwa njia ya Rubavu-Kigali-Rusumo kuelekea Wilaya ya Chato kaskazini-magharibi mwa Tanzania.





Post a Comment

Previous Post Next Post