Na Mwandishi wetu –SHINYANGA
Mwenyekiti wa Umoja wa
wanawake Tanzania U.W.T CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Bi
Rehema Nhamanilo ameonya wanachama wa jumuiya hiyo kuepuka kupokea
zawadi za watia nia wa nafasi za Ubunge na udiwani kwa lengo la kuwachagua
kwenye uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika baadaye mwaka huu 2025,kwani
amesema kwa kufanya hivyo ni kuhalalisha rushwa.
Nhamanilo ameyasema hayo wakati
akizungumza na viongozi na wanachama wa CCM na jumuiya zake katika kata za
Mwamalili,Old Shinyanga,Kizumbi,Ibinzamata na Ibadakuli ikiwa ni mwendelezo wa
ziara ya kamati ya utekelezaji ya U.W.T Wilaya ya Shinyanga Mjini,ambayo
imelenga kukagua uhai wa Chama.
Amesisitiza viongozi na wanachama
kuepuka kupokea zawadi za watia nia wa nafasi za uongozi kwenye uchaguzi
Mkuu baadaye Mwaka huu,na badala yake wanapaswa kuwa mfano na kielelezo cha
uadilifu kwa kuzingatia miiko ya chama hicho,na kuongeza kuwa kwa kushiriki
vitendo hivyo inachangia kurudisha nyuma maendeleo.
Amekemea pia kuhusu tabia ya
kuchafuana na kudhoofishana kisiasa hasa katika kipindi hiki cha kuelekea
kwenye Uchaguzi Mkuu wa Rais,wabunge na madiwani,na badala yake waendelee
kushirikiana na kuimarisha umoja na mshikamano miongoni mwao,kwani ndiyo
silaha ya ushindi.
Ametahadharisha kuepuka kampeini
kabla ya wakati kwani kwa kufanya hivyo ni fujo na ukiukaji wa maadili ya
Chama lakini pia ni kuwakatisha tamaa na kuwadhoofisha kisaikolojia wabuge na
madiwani waliopo madarakani,ambapo ametaka waachwe wakamilishe kipindi chao
kilichobaki, na amesisitiza kuhusu misingi ya utu,heshima na
ubinaadamu,”waacheni wafanye kazi,wakamilishe kipindi chao
kilichobaki,msiwabeze viongozi waliopo madarakani,wasipuuzwe, subirini
wakati wa kampeini utakapofika kuliko kuanza sasa”
Mwenyekiti huyo wa UWT Wilaya ya
Shinyanga Mjini amesema wakati utakapofika wanachama hao hasa wanawake
wachukue fomu za kugombea ubunge na udiwani,kwani hiyo ndiyo demokrasia.
Kwa upande wake katibu wa UWT –CCM
wilaya ya Shinyanga Mjini Bi Getrude Mboyi amewakumbusha viongozi wa kata na
matawi kuwajibikia jukumu la kusimamia uhai wa chama na wanachama
kuhakikisha wanalipa ada ili kuendelea kuimarisha uimara wa CCM na
jumuiya zake.
Katika ziara hiyo wajumbe wa kamati ya
utekelezaji ya UWT wilaya ya Shinyanga Mjini wamewasilisha mada za maadili na
uchaguzi,ukatili wa kijinsia,mahusiano na ushirikiano na jamii.
Ziara hiyo iliyoanza tangu Mei
12,2025 inatarajiwa kuhitimishwa Mei 19,2025 ambapo viongozi hao wa UWT wilaya
ya Shinyanga mjini watatembelea katika kata zote, na tayari viongozi hao
wamekwishatembelea kata za Ibadakuli,Kizumbi,Ibinzamata,

Post a Comment