Na Mapuli Kitina
Misalaba
Katibu Tawala Msaidizi
wa Mkoa wa Shinyanga, David Lyamoga,
akizungumza kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa ambaye alikuwa mgeni rasmi,
ametoa wito kwa jamii kuwekeza kikamilifu katika malezi na makuzi ya watoto ili
kujenga msingi imara wa familia na taifa kwa ujumla.
Lyamoga
ametoa kauli hiyo leo Mei 15, 2025, katika mdahalo ulioandaliwa kwa ajili ya
kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya
Familia, ambapo Tanzania huungana na mataifa mengine duniani kutafakari
nafasi ya familia katika ustawi wa jamii.
“Nichukue
fursa hii ya kipekee kuwashukuru waandaaji wa kongamano hili muhimu la kujadili
masuala ya malezi na familia. Kaulimbiu ya mwaka huu inasema ‘Mtoto ni
Malezi: Msingi wa Familia Bora Taifa Imara’, ikitukumbusha kwamba
tusipojenga misingi bora ya familia kupitia malezi mazuri ya watoto wetu,
hatuwezi kuwa na taifa imara,” amesema Lyamoga.
Ameongeza
kuwa serikali kupitia Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo
ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM) imejikita katika maeneo matano muhimu: afya bora,
lishe, malezi yenye mwitikio, fursa za ujifunzaji wa awali, na ulinzi na
usalama.
Lyamoga
amesisitiza kuwa changamoto nyingi zinazolikumba taifa zikiwemo mmomonyoko wa
maadili na ukatili dhidi ya watoto zinatokana na udhaifu wa malezi kuanzia
ngazi ya familia. “Ni matumaini yangu maazimio yatakayopatikana hapa
yatawasilishwa serikalini na pia kuingia kwenye kongamano la kitaifa la Malezi
Summit Mei 23-24 mwaka huu,” amesema.
Kwa
upande wake, Mganga Mkuu wa Mkoa wa
Shinyanga Dkt. Yudas Ndungile amewakumbusha wazazi na walezi kuhakikisha
watoto wao wanapata malezi bora ili taifa lipate kizazi chenye maadili na afya
njema.
Naye
Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa, Lydia
Kwesigabo, ametaja baadhi ya maazimio ya mdahalo huo kuwa ni:kuwe na
uendelevu wa midahalo kuhusu masuala ya malezi,
Kuendelea kutoa elimu kwa jamii, wazazi na walezi
kuhusu malezi ya watoto,Kufikisha elimu hiyo hadi katika vyuo mbalimbali.
Afisa Maendeleo ya Jamii wa Mkoa, Christina Gunje, amekemea vikali mmomonyoko wa maadili unaoanzia
katika familia ambapo amesema familia nyingi hazina utaratibu wa kuzungumza na
watoto wao, hali inayochangia watoto kukosa maarifa sahihi ya maisha.
Gunje ameonya pia juu
ya ukatili wa watoto kupitia mitandao ya kijamii, akisisitiza kuwa wazazi wawe
makini na matumizi ya teknolojia kwa watoto.
Baadhi
ya washiriki wa mdahalo huo wamechangia maoni mbalimbali kuhusu njia bora za kuimarisha
malezi, wakisisitiza elimu ya mara kwa mara kwa wazazi na ushirikishwaji wa
jamii kwa ujumla.
Mdahalo huo
umehudhuriwa na wadau mbalimbali wa maendeleo, wataalamu wa afya, elimu na
ustawi wa jamii.
Mdahalo huo
umehudhuriwa na wawakilishi kutoka: Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa, Sekretarieti ya Mkoa wa Shinyanga na Manispaa ya Shinyanga,
Kamati ya Amani ya Mkoa, Viongozi wa dini, Watendaji
wa Kata na Wenyeviti wa Mitaa wa Manispaa ya Shinyanga, Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa (RPC), Waandishi wa masuala ya malezi kutoka Klabu ya Waandishi wa
Habari Mkoa, Shirika la ICS linalojihusisha na
malezi ya watoto, Mitandao ya SHY EVAWC,
SMAUJATA na Chama cha Wanaume Mkoa, Umoja wa
vituo vya malezi ya watoto wadogo na makao ya watoto, Baraza la Wazee Mkoa na Baraza la Watoto Mkoa, Wawakilishi wa watu wenye ulemavu, vijana, wanawake na watoa
huduma ngazi ya jamii kupitia shirika la Justwai, Wanafunzi kutoka vyuo vya Serikali za Mitaa – Hombolo na SHYCOM.

Katibu Tawala Msaidizi
wa Mkoa wa Shinyanga, David Lyamoga,
akizungumza kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa.
Katibu Tawala Msaidizi
wa Mkoa wa Shinyanga, David Lyamoga,
akizungumza kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa
Shinyanga Dkt. Yudas Ndungile.
Post a Comment