Kiongozi wa ubunifu na mikakati na msimamizi wa chapa kampuni ya jambo Group NICKSON GEORGE akizungumza
Na Suzy Butondo, Shinyanga
Kiongozi wa ubunifu na mikakati na msimamizi wa chapa kampuni ya jambo Group NICKSON GEORGE amewataka vijana kutumia majukwaa mbalimbali kuonesha vipaji vyao ili waweze kuvitumia na kujipatia kipato, wasikae na kujibweteka wakitegemea kuajiliwa na kushindwa kufikia ndoto zao na wengine kujiunga na makundi maovu.
George ameyasema wakati wa kampeni maalum ya mimi mwamba iliyolenga kuibuwa vipaji, mbalimbali kwa vijana, ambapo amewaomba wazazi kuacha kuwaficha watoto wao ili wafikie ndoto zao.
"Kampuni ya jambo mara nyingi imekuwa ikiitisha matamasha ya kuibua vipaji mbalimbali vya watoto, na leo imezindua kampeni maalumu ya mimi Mwamba ambayo imelenga kuibua vipaji malimbali vya vijana niwaombe sana wazazi muwaruhu vijana wawe wanajitokeza kwenye matamasha haya "amesema George.
Aidha baadhi ya vijana waliojitokeza kuonesha vipaji vyao akiwemo Idd Sima,msanii wa muziki Yona Msi msanii wa nyimbo, Chita Boy mbunifu wa mitindo na Elias Nyanda wameishukuru kampuni ya jambo group kwa hatua ambayo imewezesha kuwaibuwa vijana wengi ambao vipaji vyao vilikuwa vimejificha.
Katika tamasha hilo vijana mbalimali walionyesha vipaji vyao ambapo washindi walipatiwa zawadi mbalimbali, walionyesha vipaji mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuimba, kucheza, kupiga danadana, pamoja na kushiriki mashindano ya kula ugali,mikate, na kuvuta kamba.
Post a Comment