Aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba Mhe. Humphrey Polepole ameitisha Mkutano na Waandishi wa Habari siku ya tarehe 17 Julai 2025, saa 5 asubuhi.
Polepole ametoa wito huo kupitia akaunti yake ya instagram, ambapo amesema kuwa ataifafanua barua aliyomuandikia Mhe. Rais kwa hatua na kwa maana njema ili kuondoa upotoshaji.
Polepole amekanusha kutafuta maisha nje ya Tanzania, na kusema “jambo hilo halipo katika fikra zangu za jana, leo na kesho.”Polepole akanusha madai ya kuomba hifadhi nje ya nchi: Kuondoka Tanzania ni jambo ambalo sitokaa nilifanye.👇
Post a Comment