Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Edwin Mhede (kulia) akiongoza zoezi la uchanjaji wa mifugo (kuku) alipotembelea wafugaji wa mkoa wa Njombe Julai 04, 2025, ikiwa ni muendelezo wa zoezi la uhamasishaji utoaji chanjo na utambuzi wa mifugo iliyofanyika katika Wilaya ya Makete, mkoani Njombe.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Edwin Mhede akisikiliza changamoto mbalimbali zinazowakabili wafugaji Halmashauri ya Mji wa Njombe kutoka kwa baadhi ya wafugaji waliojitokeza kuchanja na kutambua mifugo yao alipotembelea wafugaji wa Halmashauri hiyo Julai 04, 2025 ikiwa ni muendelezo wa zoezi la uhamasishaji utoaji chanjo na utambuzi wa mifugo iliyofanyika katika Mtaa wa Lunyani, Wilaya ya Njombe mkoani Njombe.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Edwin Mhede akipata maelezo kuhusiana na uendeshwaji wa zoezi la uchanjaji na utambuzi wa mifugo kutoka kwa Daktari wa Mifugo Halmashauri ya Mji wa Njombe Dkt. Godphrey Kongo alipotembelea wafugaji wa Halmashauri hiyo Julai 04, 2025 ikiwa ni muendelezo wa zoezi la uhamasishaji utoaji chanjo na utambuzi wa mifugo iliyofanyika katika Mtaa wa Lunyani, Wilaya ya Njombe mkoani Njombe.