" BAWACHA MARA WACHANGIA MILIONI 1 KWA AJILI YA UJENZI WA UKUMBI WA CHADEMA KANDA YA SERENGETI

BAWACHA MARA WACHANGIA MILIONI 1 KWA AJILI YA UJENZI WA UKUMBI WA CHADEMA KANDA YA SERENGETI

Baraza la Wanawake wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAWACHA) Mkoa wa Mara wamechangia kiasi cha Shilingi 1,000,000 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa ukumbi wa vikao wa Ofisi ya CHADEMA Kanda ya Serengeti.

Mchango huo umekabidhiwa na Mwenyekiti wa BAWACHA Mkoa wa Mara, Veronica Sando, kwa niaba ya wanawake wote wa BAWACHA Mkoa wa Mara.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Bi. Veronica amesema kuwa BAWACHA kupitia vikao vyao imeamua kuunga mkono juhudi za ujenzi wa ukumbi huo ili kuhakikisha chama kinakuwa na kumbi zake wenyewe kwa ajili ya shughuli mbalimbali pamoja na vikao vya chama.

Aidha, amesema kuwa mchango huo ni sehemu ya dhamira ya wanawake wa BAWACHA katika kuimarisha miundombinu ya chama na kuendelea kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya kisiasa na kijamii ndani ya chama hicho.

Tukio la kukabidhi mchango huo limefanyika katika Jimbo la Kahama Mjini wakati wa maandalizi ya mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika jana, ambapo maelfu ya wananchi walihudhuria mkutano huo.

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

 

Post a Comment

Previous Post Next Post