" TAMESOT YATOA TAMKO KWA WARATIBU WA SERIKALI

TAMESOT YATOA TAMKO KWA WARATIBU WA SERIKALI

Na Mwandishi wetu, Misalaba Media

Chama cha waganga wa tiba asili  TAMESOT kimetoa wito kwa waratibu wa serikali kitengo cha afya  kikiwaomba ushirikiano wakuwafikia waganga wa tiba asili katika kutoa elimu ya uhamasishaji juu ya ushiriki wa wiki ya tiba asili ya mwafrika.


Ameyasema hayo Katibu mkuu wa chama hicho  Lukas Joseph Mlipu   akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Geita  kwa lengo la kukutana na waganga wa tiba asili  ambapo amesema chama hicho kimeanza ziara yakuwa fikia wanga maeneo mbalimbali ili kuwaeleza umuhimu wa kushiriki maadhimisho hayo ambayo yametambuliwa na serikali. 
 
"Tunaipongeza serikali yetu tukufu kuiweka siku hii maalumu kwa waganga wa tiba asili wa Mwafrika, kwani siku hii inatambua tiba asili ya mwafrika na kuifanya kufahamika kwa Dunia nzima  kuwa zipo dawa za asili zinasaidia katika kutibu magonjwa mbali mbali yakiwemo  magonjwa ya kuambukizwa na yasiyo ya kuambukizwa pamoja  na magonjwa ya mlipuko,
siku hii inaheshimisha Taaluma hii na nchi yetu katika Eneo zima la ulimwengu" amesema katibu mkuu Lukas Mlipu.

Hata hivyo ameeleza kusikitishwa na baadhi ya waratibu wa halmashauri  kutoka kitengo cha afya wanaojaribu kukwamisha viongozi wa TAMESOT kwa baadhi ya wilaya akama ambavyo ametolea mfano wa halmshauri ya wilaya Misungwi mkoa Mwanza  baada ya kupokea taarifa kutoka kwa viongozi wa chama  wakilalamika  kukwamishwa katika zoezi la utoaji barua za utambulisho juu ya  kuwahamasisha waganga kushiriki ziara ya Katibu mkuu huyo Lukas Mplipu.

 "Tunomba ushirikiano kwa waratibu wa tiba asili na tiba mbadala wa Halmashauri zote nchini  Tanzania bara  baadhi yao wamekuwa kikwazo kwa  vyama tunahitaji kusonga mbele bila ya vikwazo." ameendelea kusisitiza katibu mkuu Lukas.

 Amefafanua kwamba tayari serikali imewatambulisha   wajumbe 15 kwa mwaka huu wakiwemo na viongozi wa vyama vya tiba asili na tiba mbadala watakaoshiriki   kikamilifu katika hamasa  ya ushiriki wa wiki ya tiba asili ya mwafrika itakayo fanyika mkoani Dodoma  kuanzia tarehe 25 hadi 31/ 08/ 2025:

Ziara ya Katibu Mkuu inalenga uhamasishaji  waganga mikoa 15 ukiwemo mkoa Kagera  akiwa ameanzia mkoa wa Geita tangu Tarehe
14/07/2025.

Katika uhamasishaji ameishakamilisha mikutano  yake  wilaya ya Bukombe na Leo yupo wilaya ya Chato, na tarehe 19/08/2025 atakuwa wilaya ya Geita mjini na kuhitimisha ziara yake wilaya ya Nyangh'wale Mkoani Geita.

Aidha ziara yake itaendelea Mkoani Mwanza  Tarehe 21hadi 22/08/2025 wilaya ya Ilemela  kata ya Igombe B Kabla ya katibu Mkuu huyo kuelekea Mkoa wa Mara kwa ziara  ya siku 2 ambapo tarehe 26 -28/08/2025 atakuwa Mkoani Kagera , Halmashauri ya Manispaa  ya Bukoba  

 Ametoa  wito kwa waganga wasisite  kushiriki maadhimisho hayo yenye fursa mbalimbali kwao.

Post a Comment

Previous Post Next Post