" MKURUGENZI WA TAASISI YA ROCKEN HILL NA ANDERLEK AWASISITIZIA WAZAZI KUIMARISHA MAADILI YA WATOTO

MKURUGENZI WA TAASISI YA ROCKEN HILL NA ANDERLEK AWASISITIZIA WAZAZI KUIMARISHA MAADILI YA WATOTO

Na  Neema Sawaka, KahamaMkurugenzi wa taasisi za  Rocken Hill na Anderlek Ridges  iliyopo  Manispaa ya Kahama   Mkoani Shinyanga Alexander Kazimil amewashauri wazazi  kutochoka katika kufundisha matumizi mazuri ya teknolojia  yanayoendelea kuwepo  na kuepukana na Matumizi  ya madawa ya kulevya kwa vijana.Kazimil  amesema hayo katika Mahafali ya 21 ya darasa la saba na  Mahafali ya 17 ya kidato cha nne  huku akieleza mtoto akimaliza kidato cha nne sio  kumuachaniza kwa madai amekuwa  bila kumkumbushia  maadili na malezi mema na nidhamu katika jamii.Kazimil amesema tecknolojia ni nzuri nani mbaya haiwezi kukwepeka kwa watoto hivyo jitihada zinahitajika kwa wazazi,walimu na jamii nzima kuhakikisha watoto wanapata malezi na kuwakumbusha kila siku kutotumia madawa ya kulevya."Muwaeleze watoto kuwa wavumilivu kwani  maisha yanaweza kuwa juu au chini nakutambua vipaji walivyonavyo  ambavyo vitawasaidia kujipatia ajira na kuendeleza maisha yao"amesema Kazimil.Kazimil amesema vijana wanatakiwa kuandaliwa kiimani na kimaadili  kwani wapo wazazi wengine wamekuwa wakilea watoto wao kama mabosi kwa kuogopa hata kuwatuma kazi majumbani kwani wakifanya hivyo wataweza kutengeneza kizazi kisicho bora hapo baadaye.Kazimil amesema   elimu siyo ya kuchezea na kwani ndiyo inayoendesha maisha haimuondolei mtu umasikini bali inamtaka kila mmoja kujifunza na kupambana na wimbi la umasikini na watu wasiwakatishe tamaa.Mkurugenzi wa  Shule za msingi  Rocken Hill  Dkt Zephania Madaha amesema    shule hizo  zinawahitimu 186 wa darass la saba zimekuwa zikifundisha  masuala ya Mshikamano,maadili na imani  kwani wameona dunia inavyokwenda na kuwataka wawe na hofu ya mungu ili waweze kutimiza ndoto zao.Naye  Mkurugenzi wa shule ya Anderlek Ridges Godwin Ng'osha  amesema wamekuwa wakifanya viziri kitaaluma nakuwapongeza wazazi  kwa kuwaamini kuwa na watoto wao muda wote kwa kipindi cha miaka minneMgeni rasmi katika mahafali hayo katibu  wa baraza la  ushauri la wazee. Anderson Lyimo amesema  watoto wasipolelewa vizuri watamomonyoka kimaadili nakuwa taifa la watu wa hovyo hivyo mafundisho mema yaendelee ndani ya familia ili nchi iwe ya amani na utulivu hasa kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu.mwisho.

Post a Comment

Previous Post Next Post