" RAIS SAMIA KUKATA KIU YA WANANCHI MKOANI MBEYA AAHIDI MIRADI MIPYA NA KUENDELEZA ALIPOFIKIA KWA MIAKA MITANO

RAIS SAMIA KUKATA KIU YA WANANCHI MKOANI MBEYA AAHIDI MIRADI MIPYA NA KUENDELEZA ALIPOFIKIA KWA MIAKA MITANO

Na Lydia Lugakila 

Mbeya 

Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi CCM na mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta Samia Suluhu Hassan amesema bado ana kiu kubwa ya kuwaletea maendeleo Watanzania hasa wananchi wa mkoa wa Mbeya katika kuwaletea maendeleo kupitia miradi mipya na kuendeleza alipofikia kwa kipindi hiki .

Dokta Samia ametoa kauli hiyo Agosti 4, 2025 katika mkutano wa kampeni za kuwania  Urais wa Jamhuri y Muungano wa Tanzania uliofanyika katika Uwanja wa Ndege wa Zamani (Old Airport) mkoani Mbeya lengo likiwa ni kuwashukuru wananchi kumuamini.

Dokta Samia amesema kuwa endapo atapata nafasi ya kupeperusha bendera ya chama hicho atahakikisha anaendeleza miradi mipya na kufanya mwendelezo wa miradi iliyopo.

Amesema serikali inakwenda kutenga fedha za mfumo maalum kwa kugharamia matibabu ya vipimo muhimu vya maradhi kwa Wananchi wasiokuwa na uwezo hasa katika magonjwa ya saratani, Figo, moyo kisukari,mishipa ya fahamu kutokana na magonjwa hayo kugharamia fedha nyingi.

Rais Samia ameongeza kuwa serikali itahakikisha pia inaweka mazingira mazuri katika sekta ya afya huku akieleza kuwa  ajenda kubwa kuelekea 2030 ni kufanya kilimo kukua kwa asilimia 10 kutoka asilimia 4.6 iliyopo kwa sasa.

 Aidha Dokta Samia amewashukuru wananchi mkoani Mbeya kwa mapokezi na hamasa kubwa Mkutano wa kampeni za Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM)uliofanyika katika Uwanja wa Ndege wa Zamani (Old Airport) mkoani Mbeya.

Amesema kuwa wananchi hao waliojitokeza  kwa wingi katika mkutano huo wameonyesha hali ya  kumpa moyo na imani ya ushindi wa kishindo.

Amesema kuwa endapo akipata ridhaa ya kupeperusha bendera ya chama cha mapinduzi (CCM) atafanya yote yanayowezekana ambapo katika sekta ya kilimo Ifikapo 2030  kilimo kitakua  kwa asilimia 10 kutoka asilimia 6.4 iliyopo kwa sasa ambapo pia amewashukuru wakulima wote kwa kufanya biashara ya chakula kuimarika na  kuahidi kuweka kongani ya vijana ili kuwawezesha kujiajiri wenyewe.

Hata hivyo amesema atahakikisha  kujenga daraja la kuvusha watu maeneo ya mwanjelwa Mkoani humo ili kuondoa adha waipatayo wananchi.

Ameomba wana Mbeya kumuunga mkono kwa kumpigia kura za kutosha ili kufanikisha kupata nafasi hiyo na kuwaongoza Watanzania.

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

Post a Comment

Previous Post Next Post