" STAND UNITED KUFANYA TAMASHA LA SIKU YA WANA 'YES! YES! YES! OKTOBA 04, 2025.

STAND UNITED KUFANYA TAMASHA LA SIKU YA WANA 'YES! YES! YES! OKTOBA 04, 2025.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi, Ndg. Chrispin Kakwaya akitoa taarifa kwa vyombo vya habari juu ya tamasha la Stand United Oktoba 4, 2025 litakalofanyika uwanya wa CCM Kambarage Manispaa ya Shinyanga

Na. Elias Gamaya – Shinyanga

Timu ya Stand United inatarajia kufanya Tamasha la Siku ya Wana Oktoba 4, 2025 katika Uwanja wa CCM Kambarage, Manispaa ya Shinyanga, ambapo mbali na burudani mbalimbali, pia kutafanyika utambulisho wa wachezaji wapya waliounganishwa kwa ajili ya msimu mpya wa Ligi ya Championship.

 Akizungumza leo Septemba 25, 2025 na vyombo vya habari kuhusu maandalizi ya tamasha hilo, Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi, Ndg. Chrispin Kakwaya, amesema lengo la tamasha ni kuwapa burudani mashabiki wa timu hiyo na kuendelea kuimarisha mshikamanano wa Stand United na wapenzi wake.

 “Tamasha litaanza saa 2 asubuhi hadi saa 12 jioni. Tutakuwa na mashindano ya mbio za baiskeli kwa wanaume na wanawake, michezo ya utangulizi ikiwemo mechi za Bajaji vs Bodaboda, Soko Kuu vs Soko la Majengo, na dabi ya Upongoji FC dhidi ya Ibinzamata,” amesema Kakwaya.

 Mbali na michezo hiyo, alisema  kutakuwa na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali wa Kanda ya Ziwa na Shinyanga. Kilele cha tamasha kitakuwa ni utambulisho wa wachezaji wapya wa Stand United kisha kufuatiwa na mtanange wa kirafiki kati ya Stand United na timu mojawapo ya Ligi Kuu Tanzania Bara ambayo itatajwa hivi karibuni.

 Kwa upande wake, Msemaji wa Stand United, Ramadhan Zorro,amesema kiingilio katika tamasha hilo kwa mzunguko sh.5,000,VIP Sh.10,000 na VVIP watakuwa na kadi maalum huku akitamba kuwa tamasha hilo litakuwa la aina yake tofauti na Matamasha mingine yaliyotanguliwa kutoka kwa Timu zingine, na kutoa wito kwa wananchi waje kwa wingi kuona kikosi ambacho wamekisajiliMsemaji wa Stand United, Ramadhan Zorro akielezea kuhusu Tamasha la Siku ya Wana 'Yes! Yes! Yes!


 

 

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

Post a Comment

Previous Post Next Post