
TANGAZO LA KAZI – MSAIDIZI WA OFISI
UTANGULIZI
Tanzanian Youth and Children (TYC) ni Asasi Isiyo ya Kiserikali (NGO).
Asasi hii ilianzishwa kama CBO mwaka 2017 na ilisajiliwa kikamilifu Aprili,
2022 na kupewa mamlaka ya kufanya kazi Tanzania Bara. Lengo letu ni kukuza na
kutetea jamii ili kuhakikisha familia zao zinakuwa huru na vikwazo vya kijamii
na kiuchumi na kufikia uwezo wao kamili katika maisha yao.
TYC inatafuta Msaidizi wa Ofisi atakayehusika na
shughuli za kila siku za uendeshaji. Ikiwa unaona unaweza kushiriki katika
majukumu yaliyotajwa, unakaribishwa kujiunga na timu yetu.
MSAIDIZI WA OFISI:
- Idadi
ya nafasi: Moja (1)
- Eneo
la kazi: Manispaa ya Shinyanga
- Mshahara:
Kifurushi cha kuvutia
Msaidizi wa ofisi atakuwa na jukumu la kufanya kazi
mbalimbali za kiutawala na za kiofisi kusaidia shughuli za kila siku.
Majukumu na Wajibu
- Kusimamia
kazi za kiofisi kama kupanga na kutuma barua pepe/nyaraka
- Kuhifadhi
na kuorodhesha vifaa vya ofisi na kuagiza vipya inapohitajika
- Kuwakaribisha
wageni ofisini
- Kujibu
simu
- Kuhakikisha
ofisi inaendeshwa kwa ufanisi
- Kupanga
ratiba za mikutano na kutuma mialiko ya vikao kwa washiriki
- Kuwakilisha
na kuhudhuria mikutano kwa ajili ya kuchukua kumbukumbu/makabrasha ya
kikao
- Kufanya
shughuli nyingine yoyote rasmi zitakazoelekezwa na msimamizi/mwajiri
Sifa na Vigezo vya Mwombaji
- Elimu
ya kuanzia kidato cha nne na kuendelea katika masomo ya Uhazili, Maendeleo
ya Jamii, Rasilimali Watu, Mipango ya Miradi, Kazi za Jamii, Teknolojia ya
Habari au fani nyingine zinazohusiana.
- Awe
na uwezo wa kufanya kazi nyingi kwa wakati mmoja na kuwa na nidhamu ya
kupanga ratiba za watu wengine.
- Uwezo
wa kompyuta za msingi
- Uwezo
wa kubadilika na kuweka vipaumbele kwenye kazi mpya zinapojitokeza
- Uwezo
wa mawasiliano ya kijamii
- Ujuzi
wa usimamizi wa muda
- Ustadi
wa kuhudumia wateja
ANGALIZO:
Usilipe fedha yoyote kwa tangazo hili. TYC inakataza aina yoyote ya rushwa
kuhusiana na nafasi hii. Tunaamini katika uadilifu, uwezo na ubunifu wa
waombaji.
Tuma barua ya maombi, CV na vyeti vya kitaaluma kabla
ya tarehe 30 Septemba, 2025. Ni waombaji walioteuliwa pekee watakaowasiliana.
Wanawake wanahimizwa kuomba wenye umri wa miaka 18
hadi 27. Tunakubali maombi kwa njia ya mtandao pekee kupitia barua pepe.
Waombaji wanaoishi Shinyanga watapewa kipaumbele.
Tuma kupitia barua pepe:
tycnew@gmail.com
Anuani:
Mkurugenzi Mtendaji
Tanzanian Youth and Children (TYC)
S.L.P 1362, Shinyanga-
Tanzania
Post a Comment