" DKT. MARGARETH NDONDE ASIMIKWA KUWA MCHUNGAJI SHEMASI DAYOSISI YA SHINYANGA.

DKT. MARGARETH NDONDE ASIMIKWA KUWA MCHUNGAJI SHEMASI DAYOSISI YA SHINYANGA.

Askofu wa Dayosisi ya Shinyanga, Mhashamu Johnson Japheth Chinyong'ole, amemsimika Dkt. Margareth Aidan Ndonde katika daraja takatifu la ushemasi, katika ibada maalumu iliyofanyika katika Kanisa la Anglikana Mtakatifu Andrew Kitangili, Dayosisi ya Shinyanga.

 Dkt. Margareth, ambaye pia ni Katibu wa UMaki na mratibu wa shughuli za maendeleo ya wanawake na watoto ngazi ya taifa, amepokea daraja hilo kama hatua muhimu ya kulitumikia Kanisa na jamii kupitia wito wake wa kichungaji.

 Akizungumza wakati wa ibada hiyo, Askofu Chinyong'ole amesisitiza umuhimu wa wachungaji kutanguliza unyenyekevu, utii na upendo katika utumishi wao huku akibainisha kuwa kazi ya kichungaji ni dhamana ya kiroho yenye uzito mkubwa kwa waamini na jamii kwa ujumla.

 “Huduma ya kichungaji si cheo, bali ni mwito wa kujitoa, kubeba mizigo ya wengine na kuwa mfano wa imani. Mungu awasaidie muwe taa na chumvi ya dunia,” amesema Askofu Chinyong'ole.

 Kwa upande wake Dkt. Margareth amehidi kulitumikia Kanisa kwa bidii, uadilifu na moyo wa kujitolea ili kuendeleza gurudumu la injili na kuinua huduma za Kanisa kwa wanawake, watoto na jamii kwa ujumla.

 “Ninaipokea dhamana hii kwa moyo wa shukrani na unyenyekevu. Nitafanya kazi kwa ushirikiano, upendo na uaminifu ili nione injili ikisonga mbele,” amesema Shemasi Dkt. Margareth.

 Naye Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Mtakatifu Andrew Kitangili, Joan Ndabakubije, amempongeza Askofu Chinyong'ole kwa kuendelea kuwaamini wachungaji wanawake, huku akisema kitendo hicho kinaimarisha imani na kuhamasisha wanawake wengi zaidi kujitoa katika huduma za uinjilisti.

“Tunaishukuru Dayosisi kwa kutuamini kama wanawake. Tutaendelea kufanya kazi kwa bidii na uaminifu ili kustahili imani hii na kuthibitisha kuwa wanawake pia wanaweza kulitumikia Kanisa kwa ufanisi na ushupavu,” amesema Mch. Ndabakubije.



























 

 

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

Post a Comment

Previous Post Next Post