Abiria wanaosafiri masafa marefu nyakati za usiku wamepatiwa elimu ya kuheshimu Sheria za usalama barabarani wawapo ndani ya gari.
Akitoa elimu hiyo Askari Polisi wa Kikosi Cha usalama barabarani Mkoa wa Shinyanga Sajenti David Ndimila amewataka Abiria kuacha tabia ya kunywa pombe kupita kiasi wawapo safarini kitu kinachowapelekea kuwa wasumbufu ndani ya Basi ikiwa ni pamoja na kumbugudhi dereva akiwa anaendesha gari.
Sajenti Ndimila amewaeleza Kuwa baadhi ya abiria wanaokuwa wamelewa wanakuwa na tabia ya kutaka kushuka kujisaidia mara kwa mara kisha kumsumbua dereva Kwa kauli za kukera kitu kinachompelekea dereva kukosa umakini akiwa anaendesha gari
Abiria wameaswa kuwa mabalozi wa usalama barabarani kwa kukemea na kuzuia vitendo hivyo visitokee ndani ya gari hasa nyakati hizo
za usiku kwani vitendo hivyo vinahatarisha usalama wa safari yao na watumiaji
wengine wa barabara.
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254


Post a Comment