" KAMATI YA SIASA YA NYAMAGANA YAWATAKA WANANCHI KUCHUKUA TAHADHARI

KAMATI YA SIASA YA NYAMAGANA YAWATAKA WANANCHI KUCHUKUA TAHADHARI


BAADA ya Mvua kubwa kunyesha Jana jijini Mwanza Tarehe11/3/2026 Na kusababisha Maafa Ikiwemo Magari kubebwa na Maji Maeneo ya Mkuyuni Diwani wa kata ya Nyamagana Dk wambura Chacha kwa kushirikiana na Kamati ya Siasa wamefanya ziala ya kukagua Miundo Mbinu ya kata ya Nyamagana. 

Akizungumza na Chombo hiki cha Habari Chacha Amesema lengo kubwa ni kutoa Tahadhari kwa wananchi wa Kata hiyo kuwa makini katika kipindi hiki cha mvua zinazoendelea kunyesha mkoani humo. 

Naye Mwenyekiti wa Mtaa wa Nyamagana Mashariki amempongeza diwani wa kata hiyo kwa kuguswa kuwatembelea baadhi ya wananchi waliopata madhara na kuona hali halisi.


Post a Comment

Previous Post Next Post