" SOKO LA NGOKOLO MITUMBANI MANISPAA YA SHINYANGA KILIO KWA WAJASIRIAMALI

SOKO LA NGOKOLO MITUMBANI MANISPAA YA SHINYANGA KILIO KWA WAJASIRIAMALI

 

Katibu wa Soko la Ngokolo Mitumbani.


Na Edington Mukiza Ezron, Misalaba Media

Baadhi ya wajasiriamali wa soko la Ngokolo mitumbani Manispaa ya Shinyanga wameeleza changamoto zinazowakabili na kuiomba serikali kuwaboreshea miundombinu ya soko hilo ili kuwaepusha na usumbufu unaojitokeza.

Akizungumza na Misalaba Media katibu wa Soko hilo Bwana Charles Bitengeko Machi 12, 2026 amesema wamekuwa wakikabiliwa na changamoto mbalimbali hasa katika kipindi cha masika ikiwemo maji kutuama katika eneo la soko hilo na kusababisha aza kwa wajasiliamali na wananchi kwa ujumla.

Bitegeko amesema kuwa changamoo hizo zimesababisha upungufu wa wateja katika soko hilo na kuathiri ulipaji wa kodi kutokana na kipato cha wajasiliamali kuwa kidogo.

Pia amesema changamoto ya maji kutuama inawaathiri pia hadi akina mama wajasiliamali wa kupika chakula (Mama Ntilie) Pamoja na soko la mbonga mboga lililopo hapo Ngokolo mitumbani.

Nao baadhi ya wajasiliamali wa Nguo za mitumba wameeleza kuwa madibwi hayo yanasababisha mizigo inayoshushwa hapo kuchafuka kutokana na maji au matope yaliyopo.

Hata hivyo wameita serikali kutatua changamoto zinazowakabili kwani zimekuwa za muda mrefu na kwamba wamezifikisha kwa viongozi husika lakini hazijapatiwa ufumbuzi hali inayoendelea kuwaathiri wajasiliamali ikiwemo kushindwa kulipa kodi kwa wakati.


  

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post