Akizungumnza na Wajumbe wa Baraza la wazazi wa CCM Wilaya ya Mpanda kwenye ukumbi wa CCM Wilaya ya Mpanda kwa lengo la kuwashukuru kwa kumchagua kuwa mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini kwenye uchaguzi wa Oktoba Mwaka Jana.
Sumry amesema kuwa miradi ya maendeleo katika sekta mbalimbali ikiwemo Afya,Barabara,Elimu,Kilimo,Maji pamoja na sekta nyingine umeongeza tija kwa wananchi kwa kusogezwa huduma hizo kwenye maeneo yao.
Katika Sekta ya Barabara kwenye manispaa ya Mpanda amesema ujenzi wa barabara wa kilomita 8.49 kupitia mradi wa TACTIC ambao utekelezaji wake umeanza kwa wakandarasi kuanza kujenga kambi kwaajili ya kuanza kutekeleza mradi huo utakaonufaisha baadhi ya kata utakuwa ni mfano wa kuigwa kwa kujengwa Barabara za kisasa zitakazo pendezesha manispaa ya Mpanda kwa kwa gharama ya zaidi ya Bilioni 21.
‘’Kwenye hili namshukuru sana Rais wetu Dkt Samia suluhu Hassan mwanzoni kulikuwa na kusuasua kwa utiaji sahihi wa mkabata huu lakini kabla ya uchaguzi wakati wa Kampeni Rais wetu alipokuja kuomba kura hapa Mpanda nilisimama na kumuomba kutia msukumo wa utiaji saini wa mkataba huo baada ya muda mkataba huo ulisainiwa na wakandarasi tayari wapo eneo la mradi na kazi inaendelea’’ anasema Haidary
Katika hatua nyiningine amewaomba wakazi wa Manispaa ya Mpanda kuupokea mradi huo wa barabara kwenye maeneo yao pindi utakapo anza kwakuwa ni bahati pekee waliyoipata kutoka kwa Rais Dkt Samia suluhu Hassan.
‘’Tukiwaona watalamu wetu wa ujenzi wa barabara wanaweka alama kwenye maeneo yetu huko tusishangae tufahamu ndio utekelezaji wa ujenzi wa barabara hizo umeanza’’amesema Haidary
Katika sekta ya Maji amesema mradi wa maji wa Miji 28 unaojengwa katika Kata ya Shanwe ambao unagharimu zaidi ya Bilioni 22 unakwenda kuondoa adha ya upatikanaji wa huduma ya maji kwa wakazi wa Manispaa ya Mpanda pindi utakapo kamilika.
Mradi huo ambao umefikia asilimia 55 unakwenda kuwa muarobaini kwa huduma ya maji kwa wanachi wa Manispaa ya Mpanda kwa kuondokana na tatizo la huduma ya Maji.
Katika Sekta ya Kilimo Haidary amesema serikali kuwekeza Bilioni 33 kwenye mradi wa kilimo cha umwagiliaji katika Kata ya Mwamkulu ni mkombozi mkubwa kwa wakulima wa kata hiyo na Manispa kwa ujumla.
‘’Tulifanya ziara kwenye eneo hilo la mradi wa umwagiliaji kiukweli mradi huo unaendelea vizuri umefikia asilimia 70 na kukamilika kwa mradi huu wa umwagiliaji ni mapinduzi makubwa ya sekta ya kilimo kwa wanachi wetu wa Manispa ya Mpanda’’ amebainisha Haidary
Kuhusu Sekta ya Elimu amesema serikali imetekeleza miradi mbalimbali ya ujenzi wa shule za sekondari kwa kuleta fedha nyingi kwa nyakati tofauti tofauti kwenye Manispaa ya Mpanda kubwa zaidi ni kujengwa kwa sekondari ya Wavuala ya Kanda Katavi katika Kata ya Kasokola yenye zaidi ya Bilioni 4 ambayo itaongeza chachu ya maendeleo ya sekta ya Elimu.Amewaomba Wanachi wa Manispaa ya Mpanda kuendelea kuimarisha umoja na mshikamano kwa kuwa maendeleo yanakwenda pamoja na umoja amani na mshikamano.
Katibu WA CCM WILAYA YA MPANDA Ndg. MUSA RAMADHAN MWEVI akiwasalimia wajumbe Wa Baraza la wazazi CCM Jimbo la mpanda mjini.
Mwenyekiti Wa JUMUIYA YA WAZAZI CCM WILAYA YA MPANDA Ndg. Pius Buzumalle akiwasalimia na kuwakaribisha wajumbe Wa Baraza hilo la wazazi CCM Jimbo la mpanda mjini 02/03/2026.
Katibu WA JUMUIYA YA WAZAZI CCM WILAYA YA MPANDA Ndg. JIMOTOLI JILALA MADUKA ameshiriki kikamilifu Baraza LA WAZAZI CCM WILAYA YA MPANDA katika Jimbo la mpanda mjini 02/03/2026.
Mbunge WA JIMBO LA MPANDA MJINI Ndg. HAIDARY HEMED SUMRY amewashukru wajumbe Wa Baraza la wazazi CCM Jimbo la mpanda mjini katika WILAYA YA MPANDA na Ndg. HAIDARY HEMED SUMRY ameahidi UMOJA NA MSHIKAMANO mbalimbali WA kuhakikisha JUMUIYA YA WAZAZI inasonga mbele kimaendeleo.
Wajumbe Wa kamati ya utekelezaji wazazi CCM WILAYA YA MPANDA 02/03/2026 wameshirikiki kikamilifu Baraza LA WAZAZI CCM Jimbo la mpanda mjini katika WILAYA YA MPANDA.
Wenyeviti wa JUMUIYA ya WAZAZI CCM kata, makatibu wazazi CCM kata na makatibu ELIMU, MALEZI NA MAZINGIRA CCM kata wote 02/03/2026 wameshirikiki kikamilifu Baraza la wazazi CCM Jimbo la mpanda mjini katika WILAYA YA MPANDA.
Mjumbe wa Baraza la wazazi CCM Jimbo la mpanda mjini katika WILAYA YA MPANDA Ndg. MHAGAMA amempongeza sana na kumshukru sana mbunge kwa moyo mzuri aliouonyesha kwa mapenzi mema ya kukutana na Baraza la WAZAZI CCM Jimbo la mpanda mjini katika WILAYA YA MPANDA kwa lengo la kuishukuru JUMUIYA YA WAZAZI CCM kupitia Jimbo la mpanda mjini.🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254




Post a Comment