
Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga, Donasian Kessy, akiwashukuru viongozi na wadau mbalimbali kwa ushirikiano.
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Shinyanga, tarehe 18/03/2025 imeandaa futari maalum iliyowakutanisha viongozi mbalimbali, wadau pamoja na wananchi, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha ushirikiano na kuendeleza ukaribu na jamii.Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga, Donasian Kessy, aliwashukuru viongozi na wadau kwa ushirikiano wanaoutoa katika utekelezaji wa majukumu ya taasisi hiyo.Alieleza kuwa TAKUKURU imekuwa ikifanya kazi kwa karibu na jamii kwa kutoa elimu, kufanya uchunguzi pamoja na kufuatilia matumizi sahihi ya fedha za umma.Aidha, alibainisha kuwa taasisi hiyo pia imekuwa mstari wa mbele katika kusaidia jamii kupitia miradi mbalimbali ya kijamii, akitolea mfano msaada wa mashine za watoto njiti uliotolewa katika hospitali za rufaa maeneo mbalimbali nchini.Alisisitiza kuwa futari hiyo ni sehemu ya juhudi za kuendeleza mshikamano na kuonyesha dhamira ya taasisi katika kulitumikia taifa kwa karibu zaidi na wananchi.Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili Julius Mtatiro, alimpongeza Mkuu wa TAKUKURU Mkoa kwa kuandaa futari hiyo muhimu iliyowakutanisha watu kutoka makundi mbalimbali.Alieleza kuwa hatua hiyo inaonesha namna taasisi hiyo inavyosogeza huduma zake karibu na wananchi.“Rushwa ni adui wa haki na huchelewesha maendeleo ya nchi yetu. Ni wajibu wa kila mmoja wetu kupinga rushwa kwa vitendo na kutoa taarifa pindi tunapoona viashiria vyake,” alisisitiza.Aliongeza kuwa vitendo vya rushwa, upendeleo na ukiukwaji wa haki havikubaliki, na kuwataka wananchi kuendelea kushirikiana na TAKUKURU ili kuhakikisha haki inatendeka kwa wote.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili Julius Mtatiro akizungumza.
Shekhe wa Mkoa wa Shinyanga Ismail Habibu Makusanya akizungumza.











🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

























Post a Comment