
Na Mapuli Kitina Misalaba
Wanawake wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya
(TUGHE) Mkoa wa Shinyanga wameshiriki kikamilifu maadhimisho ya Siku ya
Wanawake Duniani yaliyofanyika kimkoa katika Halmashauri ya Ushetu, Wilaya ya
Kahama, huku wakitumia fursa hiyo kuonyesha mchango wao katika maendeleo ya
jamii.
Wanawake hao walipata nafasi ya kuzungumza wakati Mkuu
wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, alipokuwa akitembelea mabanda ya
taasisi mbalimbali yaliyokuwa yakitoa elimu na kuonesha shughuli zao katika
eneo la maadhimisho hayo.
Akizungumza katika banda la TUGHE, Mwenyekiti wa
Kamati za Wanawake wa TUGHE Mkoa wa Shinyanga, Experantia Misalaba, amesema
wanawake wa kamati hiyo wanaunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuwapa kipaumbele wanawake
katika nyanja mbalimbali za maendeleo.
“Wanawake wa Kamati za TUGHE Mkoa wa
Shinyanga tunaunga mkono juhudi za Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa
kuendelea kutupa kipaumbele sisi wanawake,” amesema Misalaba.
Ameeleza kuwa wanawake wa TUGHE hushiriki katika
shughuli mbalimbali za kijamii na maendeleo ikiwemo kutoa mafunzo, warsha na
makongamano yanayolenga kuwawezesha wanawake na watumishi katika sekta ya
serikali na afya.
Aidha, amesema kamati ya wanawake ya TUGHE mkoa huo
imekuwa na utaratibu wa kufanya matendo ya huruma kila mwaka ifikapo Machi 8,
ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani kwa vitendo.
Amesema mwaka huu wanatarajia kutoa msaada wa vifaa
tiba katika Hospitali ya Iselamagazi (Nhindo) vikiwemo machela ya kusafirisha
wagonjwa, thermometers (vipima joto), mizani ya kupimia uzito, stethoscope,
mashine za kupimia shinikizo la damu (BP machine) pamoja na mashine za kupimia
sukari kwa lengo la kuboresha huduma za afya kwa wananchi.
Akizungumza baada ya kusikiliza maelezo hayo, Mkuu wa
Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, amewapongeza wanawake wa TUGHE kwa moyo
wao wa kujitolea kusaidia jamii.
“Hongereni sana kwa kuendelea kutatua
changamoto mbalimbali katika jamii kwa kufanya matendo ya huruma. Hii
inaonyesha namna wanawake wanavyoshiriki kikamilifu katika maendeleo ya jamii,”
amesema Mhita.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya
Shinyanga, Dkt. Kalekwa Kasanga, ameishukuru Kamati ya Wanawake wa Chama cha
Wafanyakazi wa Serikali na Afya (TUGHE) Mkoa wa Shinyanga kwa msaada wa vifaa
tiba walivyotoa katika Hospitali ya Iselamagazi, akisema hatua hiyo ni mchango
muhimu katika kuboresha huduma za afya kwa wananchi.
Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kimkoa
yamefanyika chini ya kauli mbiu isemayo “Haki kwa Wanawake na Wasichana: Msingi
wa Maendeleo Jumuishi Kufikia Dira ya 2050.”
Mwenyekiti wa Kamati za Wanawake wa TUGHE Mkoa wa Shinyanga, Experantia Misalaba, akizungumza.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, akitoa pongezi zake.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Dkt. Kalekwa Kasanga, akiishukuru Kamati za Wanawake wa TUGHE Mkoa wa Shinyanga.
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254













Post a Comment