Jumuiya ya Shujaa wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii
Tanzania (SMAUJATA) imetoa elimu ya maadili na kupinga ukatili wa kijinsia kwa
vijana wa kiume katika Manispaa ya Shinyanga, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya
Wiki ya Wanaume.
Elimu hiyo ilitolewa Aprili 24, 2026 kwa wanafunzi
wavulana wa Shule ya Sekondari Old Shinyanga, ambapo lengo kuu lilikuwa
kuwaandaa vijana hao kuwa walezi bora wa jamii na taifa la kesho pamoja na
kuwahamasisha kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Akizungumza katika hafla hiyo, Makamu Mwenyekiti wa
SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga, Mwarabu Akimu Mwimbili, alisema vijana wa kiume
wanapaswa kuzingatia maadili ya Kitanzania na kujiepusha na vitendo
vinavyokiuka maadili hayo. Alisisitiza umuhimu wa kutoa taarifa katika mamlaka
husika pale vitendo vya ukatili au ukiukwaji wa maadili vinapobainika.
Kwa upande wake, Katibu wa SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga,
Daniel Sibu, aliwataka vijana kuepuka tamaa na starehe za muda mfupi ambazo
zinaweza kuharibu maisha yao, akitaja baadhi ya vitendo hivyo kuwa ni pamoja na
michezo ya kubashiri na matumizi mabaya ya muda katika maeneo ya starehe.
Aidha, viongozi hao waliwaasa vijana kujiepusha na
matumizi ya dawa za kulevya pamoja na matumizi holela ya simu, wakieleza kuwa
mambo hayo yanaweza kuathiri ndoto na mustakabali wao.
Naye Kiongozi wa Idara ya Utamaduni, Makongamano na
Utalii Kitaifa, Daniel Kapaya, alisisitiza umuhimu wa vijana kuendeleza
utamaduni wa Kitanzania na kuwa na uthubutu, akieleza kuwa wao ni wazazi wa
baadaye na walinzi wa maadili katika jamii.
Kwa upande wao, baadhi ya wanafunzi walitoa wito kwa
viongozi na jamii kwa ujumla kuchukua hatua dhidi ya mienendo ya baadhi ya
wasanii wanaokiuka maadili ya Kitanzania, wakieleza kuwa tabia hizo huigwa na
vijana na kuchangia kuporomoka kwa maadili.
Hata hivyo, vijana hao walihimizwa kukataa ukatili wa kijinsia katika aina zote na kuachana na mfumo dume, wakielezwa kuwa hata baadhi ya wanaume huathirika na vitendo vya ukatili kutokana na mfumo huo.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254








Post a Comment