" MWENYEKITI MTAA WA DOME ATOA WITO KUDUMISHA AMANI NA KUJITUMA KAZINI

MWENYEKITI MTAA WA DOME ATOA WITO KUDUMISHA AMANI NA KUJITUMA KAZINI

Na Mapuli Kitina Misalaba

Mwenyekiti wa Mtaa wa Dome, Manispaa ya Shinyanga, Solomon Nalinga Najulwa maarufu Cheupe, ametoa wito kwa wakazi wa mtaa huo kuendelea kuwa mabalozi wazuri wa ulinzi na usalama ili kudumisha amani iliyopo.

Akizungumza na Misalaba Media, Najulwa amewashukuru na kuwapongeza wananchi wa mtaa huo kwa kuendelea kulinda amani na utulivu, hususan katika kipindi cha Sikukuu ya Pasaka, akisisitiza umuhimu wa kuendeleza hali hiyo katika maisha ya kila siku.

Amesema kuwa ushirikiano wa wananchi katika masuala ya ulinzi na usalama umekuwa chachu ya mafanikio ya mtaa huo, huku akiwahimiza kuendelea kushirikiana na vyombo vya dola ili kuhakikisha mazingira yanaendelea kuwa salama.

Aidha, Mwenyekiti huyo ametumia nafasi hiyo kuwataka vijana wanaotafuta ajira katika makampuni mbalimbali, hasa ndani ya Mkoa wa Shinyanga, kufika katika ofisi yake ili waweze kuandikiwa barua za utambulisho zitakazowasaidia kupata ajira kwa urahisi na kuepuka changamoto zisizo za lazima.

Sambamba na hilo, amewahimiza wakazi wa mtaa huo kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo, huku akiwataka vijana kujiepusha na makundi yasiyofaa yanayoweza kuharibu ndoto zao na mustakabali wao.

Kwa upande wao, baadhi ya vijana wa mtaa huo akiwemo Njile Kumalija na Emmanuel Mbeja, wameahidi kuendelea kuwa mabalozi wazuri wa amani na kushiriki kikamilifu katika kudumisha usalama wa mtaa huo pamoja na taifa kwa ujumla.

 SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

 
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post