
Ndg. Iddi Hassan Kimanta, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Katavi, akisaini kitabu cha wageni katika Ofisi ya CCM Wilaya ya Mpanda.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa
Katavi, Ndugu Iddi Hassan Kimanta amefanya ziara rasmi katika Wilaya ya Mpanda
tarehe 09 Aprili 2026, ikiwa na lengo la kuimarisha chama, kusikiliza kero za
wanachama pamoja na kuhimiza maendeleo ya kisiasa na kijamii katika ngazi ya
kata.
Katika ziara hiyo, Mwenyekiti Kimanta alikutana na
wajumbe wa halmashauri kuu za kata pamoja na mabaraza ya kata, ambapo
aliwasalimia na kuwapongeza kwa mchango wao mkubwa katika kufanikisha shughuli
za chama. Aidha, alitumia fursa hiyo kuwashukuru wajumbe hao kwa ushiriki wao
mzuri katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, akisisitiza kuwa ushindi uliopatikana
unatokana na mshikamano na juhudi za pamoja.
Akizungumza na wajumbe, alihimiza umuhimu wa kudumisha
umoja na mshikamano miongoni mwa wanachama, akieleza kuwa bila umoja hakuna
maendeleo ya kudumu ndani ya chama na jamii kwa ujumla. Pia alisisitiza
kuendelea kudumisha upendo na amani, ambavyo ni msingi wa ujenzi wa taifa lenye
utulivu.
Mwenyekiti huyo aliwataka viongozi katika ngazi
mbalimbali kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa uadilifu, akisisitiza
umuhimu wa uongozi bora unaozingatia maslahi ya wananchi. Katika hatua
nyingine, aliahidi kutoa vyeti vya shukrani kwa kila kata kama ishara ya kuthamini
mchango wao katika kuimarisha chama.
Aidha, aliwakumbusha wanachama kuhusu umuhimu wa
kulinda uhai wa Chama Cha Mapinduzi kwa kushiriki kikamilifu katika shughuli
zake pamoja na kuhakikisha ulipaji wa ada za uanachama unazingatiwa.
Kwa upande wa madiwani, Mwenyekiti Kimanta aliwahimiza
kusimamia maendeleo katika maeneo yao na kushirikiana kwa karibu na wanachama
bila ubaguzi wowote. Pia alisisitiza umuhimu wa kufanya kazi kwa ufanisi na
weledi ili kuleta matokeo chanya kwa wananchi.
Vilevile, Mstahiki Meya na Naibu Meya walihimizwa
kushughulikia na kutatua kero za wananchi kwa wakati, huku viongozi wote
wakikumbushwa kuzingatia mavazi ya chama kama sehemu ya utambulisho na nidhamu
ya kiitikadi.
Katika kuimarisha utendaji wa chama, makatibu wa
wilaya na kata pamoja na viongozi wa jumuiya walitakiwa kufanya ziara za kikazi
mara kwa mara ili kusimamia utekelezaji wa majukumu yao. Pia alisisitiza
umuhimu wa kusikiliza, kupokea na kutatua kero za wananchi kwa haraka na kwa
haki.
Mwisho, aligusia nafasi ya wabunge wa majimbo na wa
viti maalum kutoka mkoa wa Katavi wanaotokana na CCM, akiwahimiza kuendelea
kushirikiana na wananchi pamoja na kusimamia maendeleo ya maeneo yao.
Wajumbe wa Kamati ya Siasa Wilaya ya Mpanda wakiwa katika kikao pamoja na Ndg. Iddi Hassan Kimanta, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Katavi.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mpanda, Jimotoli Jilala Maduka.
Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda walisimama na kuwasilishwa kwa wajumbe katika kikao cha ziara ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Katavi, Ndg. Iddi Hassan Kimanta.
Katibu wa CCM Wilaya ya Mpanda, Ndg. Musa Ramadhan Mwevi, akiwasalimia wajumbe na kutoa utambulisho mbalimbali katika kikao cha ziara ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Katavi, Ndg. Iddi Hassan Kimanta, kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Mjini.
Ndg. Charles Venance Philipo, Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda, akiwasalimia wajumbe na kuwashukuru kwa kujitokeza kwa wingi kuhudhuria ziara ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Katavi, Ndg. Iddi Hassan Kimanta.
Ndg. Lwamba, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mpanda, akiwasalimia wajumbe katika kikao cha ziara ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Katavi, Ndg. Iddi Hassan Kimanta, kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Mjini leo tarehe 09/04/2026 majira ya saa 4:30 asubuhi, ambapo pia alifungua kikao kwa kuwaomba wajumbe wawe watulivu ili kusikiliza maelekezo mbalimbali.
Ndg. Amiry, Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Mkoa wa Katavi, akiwasalimia wajumbe katika kikao cha ziara ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Katavi.
Wajumbe wa Halmashauri Kuu za Kata na Mabaraza ya Kata wakiwa katika kikao cha ziara ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Katavi, Ndg. Iddi Hassan Kimanta.
Ndg. Nkana, Naibu Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda, akiwasalimia wajumbe katika kikao cha ziara ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Katavi, Ndg. Iddi Hassan Kimanta.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254













Post a Comment