Na Mapuli Kitina Misalaba
Timu ya UFUKUNYUNGU FC kutoka kata ya Ngokolo mjini
Shinyanga imefanikiwa kusonga mbele katika mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026
licha ya kupoteza mchezo wa leo kwa bao 1-0 dhidi ya MWASENGE FC kutoka kata ya
Salawe.
Katika mchezo huo uliokuwa na ushindani mkubwa ndani
ya uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa, MWASENGE FC walifanikiwa kupata ushindi wa
bao moja lakini matokeo hayo hayakutosha kuiondoa UFUKUNYUNGU FC kutokana na
hesabu ya jumla ya mabao katika michezo miwili ya mtoano.
Ikumbukwe kuwa katika mchezo wa kwanza uliochezwa kati
ya timu hizo, UFUKUNYUNGU FC waliibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya
MWASENGE FC, hali iliyowalazimu MWASENGE FC kuhitaji ushindi wa mabao 3-0
katika mchezo wa leo ili waweze kufuzu hatua inayofuata ya mashindano hayo.
Kutokana na ushindi wa leo wa bao 1-0, MWASENGE FC
wamejikuta wakiondolewa rasmi katika mashindano hayo huku UFUKUNYUNGU FC
wakifanikiwa kuendelea mbele kwa jumla ya mabao 2-1.
Kutokana na ushindi huo wa jumla ya mabao 2-1, timu ya UFUKUNYUNGU FC sasa itakutana na HOME BOYS katika hatua inayofuata ya mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 katika mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na timu zote mbili kuonesha kiwango kizuri katika michezo yao ya awali.
Baada ya mchezo huo, viongozi wa MWASENGE FC
wamemshukuru mwandaaji wa mashindano hayo Paul Daud Augustino kwa kuwapa nafasi
ya kushiriki katika mashindano hayo huku wakiahidi kurejea kwa nguvu zaidi
katika mashindano yajayo.
Kwa upande wake Katibu wa Kamati ya Mashindano Sambayi
Jilya ametangaza ratiba ya mchezo wa kesho ambapo timu ya MWANDUTU FC
itamenyana na DUARA FC katika pambano linalotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa
ndani ya mashindano hayo.
Aidha amewahimiza wananchi pamoja na mashabiki wa soka
kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa Mwabenda kuendelea kushuhudia burudani ya
soka pamoja na vipaji vya vijana vinavyoendelea kuibuliwa kupitia mashindano
hayo.
Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na Paul
Daud Augustino kupitia ufadhili wa shirika la Lushu Foundation kwa lengo la
kuibua vipaji vya vijana, kukuza michezo pamoja na kuimarisha mshikamano wa
jamii kupitia soka.
Kwa huduma za ushereheshaji wa shughuli mbalimbali, matangazo pamoja na burudani unaweza kuwasiliana na Paul Daud Augustino kupitia namba 0757 267 738.
Timu ya Mwasenge FC
Wachezaji wa UFUKUNYUNGU FC na MWASENGE FC wakioneshana ushindani mkubwa katika mchezo wa mtoano wa NIACHEKONA CUP 2026 uliochezwa uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa leo Mei 28, 2026.

Wachezaji wa UFUKUNYUNGU FC na MWASENGE FC wakioneshana ushindani mkubwa katika mchezo wa mtoano wa NIACHEKONA CUP 2026 uliochezwa uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa leo Mei 28, 2026.

Wachezaji wa UFUKUNYUNGU FC na MWASENGE FC wakioneshana ushindani mkubwa katika mchezo wa mtoano wa NIACHEKONA CUP 2026 uliochezwa uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa leo Mei 28, 2026.

Viongozi pamoja na wadau wa michezo wakifuatilia mchezo wa mtoano uliowakutanisha UFUKUNYUNGU FC dhidi ya MWASENGE FC leo Alhamisi Mei 28, 2026.

Viongozi pamoja na wadau wa michezo wakifuatilia mchezo wa mtoano uliowakutanisha UFUKUNYUNGU FC dhidi ya MWASENGE FC leo Alhamisi Mei 28, 2026.

Wachezaji wa MWASENGE FC wakipambana kutafuta mabao zaidi ya kufuzu hatua inayofuata ya mashindano hayo.

Mashabiki wakifuatilia kwa hamasa kubwa pambano kali kati ya UFUKUNYUNGU FC na MWASENGE FC katika uwanja wa Mwabenda.

Mashabiki wakifuatilia pambano kali kati ya UFUKUNYUNGU FC na MWASENGE FC katika uwanja wa Mwabenda.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254



















Post a Comment