" ASKARI POLISI SHINYANGA AHAMASISHA WAZAZI KUANZA ELIMU YA USALAMA BARABARANI NDANI YA FAMILIA KUPUNGUZA AJALI

ASKARI POLISI SHINYANGA AHAMASISHA WAZAZI KUANZA ELIMU YA USALAMA BARABARANI NDANI YA FAMILIA KUPUNGUZA AJALI

 Habari picha ikimuonesha Askari Polisi wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Shinyanga, Sajenti David Ndimila, akitoa elimu kwa wazazi kuhusu umuhimu wa kuanza kutoa elimu ya usalama barabarani ndani ya familia ili kusaidia kupunguza ajali za mara kwa mara.

Akizungumza wakati wa utoaji wa elimu hiyo, Sajenti Ndimila amewahimiza wazazi kuwa mstari wa mbele katika kuwafundisha watoto wao kanuni na matumizi sahihi ya barabara. Ameeleza kuwa kujenga utamaduni wa kutoa elimu ya usalama barabarani ndani ya familia ni mbinu muhimu ya kujikinga na ajali, kulinda maisha na kuepusha vifo pamoja na ulemavu unaotokana na ajali za barabarani.

Post a Comment

Previous Post Next Post