Madereva wa pikipiki katika Manispaa ya Kahama wamepatiwa elimu kuhusu matumizi sahihi ya taa za kuongozea magari barabarani, katika juhudi za kupunguza ajali zinazoweza kuepukika.
Elimu hiyo imetolewa na Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani Wilaya ya Kahama, Koplo Zuhura Mlungwana, katika eneo la Barabara ya Lumambo.
Koplo Mlungwana amewasisitiza madereva hao kuzingatia Sheria za Usalama Barabarani kwa kufuata ipasavyo maelekezo ya taa pamoja na alama nyingine za usalama barabarani bila kusukumwa.
Aidha, amewataka madereva wa pikipiki kuepuka kubeba mizigo inayozidi uwezo wa vyombo vyao vya usafiri, akieleza kuwa hali hiyo inaweza kusababisha kupoteza mwelekeo na hatimaye ajali.
Kwa upande wao, madereva wa pikipiki wameahidi kuzingatia elimu hiyo kwa kufuata sheria za usalama barabarani na kuwa mabalozi wazuri wa kuhamasisha wengine kutumia barabara kwa usalama wakati wote.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
Post a Comment