
Na Mapuli Kitina Misalaba
Timu ya Bulige FC imefanikiwa kumaliza katika nafasi
ya tatu ya mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 baada ya kuibuka na ushindi wa
mikwaju ya penati dhidi ya Duara FC katika mchezo wa kusaka mshindi wa tatu
uliochezwa leo Juni 23, 2026 katika Uwanja wa Mwabenda, Kata ya Solwa,
Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.
Ndani ya dakika 90 za mchezo huo, timu zote mbili
zilishindwa kufungana na kufanya mchezo kumalizika kwa sare ya bila kufungana.
Matokeo hayo yalipelekea timu hizo kwenda kwenye
mikwaju ya penalti ambapo Bulige FC ilionyesha utulivu mkubwa na kufanikiwa
kushinda kwa penalti 3-1, ushindi ulioihakikishia nafasi ya tatu katika
mashindano hayo.
Kwa ushindi huo, Bulige FC imeondoka na zawadi ya
mshindi wa tatu, huku Duara FC ikimaliza mashindano hayo katika nafasi ya nne
baada ya kuonyesha ushindani mkubwa tangu kuanza kwa michuano hiyo.
Macho ya mashabiki sasa yanaelekezwa katika mchezo wa
fainali utakaowakutanisha Ufukunyungu FC kutoka Manispaa ya Shinyanga na Kashishi
FC kutoka Kata ya Solwa, mchezo utakaoamua bingwa wa NIACHEKONA CUP 2026.
Mashindano hayo yameandaliwa na Paul Daud Augustino
maarufu MC NIACHEKONA kwa ufadhili wa Shirika la Lushu Foundation, yakilenga
kuibua vipaji vya vijana, kukuza michezo na kuimarisha mshikamano wa jamii.
Kwa huduma za MC, matangazo na ushereheshaji wa
matukio mbalimbali, wasiliana na MC NIACHEKONA kupitia namba 0757 267 738.


SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254








Post a Comment