Na Mapuli Kitina Misalaba
Timu ya Kimandaguli FC imefanikiwa kutinga hatua
inayofuata ya mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 baada ya kuibuka na ushindi wa
mikwaju ya penati 6-5 dhidi ya Kashishi FC katika mchezo wa marudiano
uliochezwa leo Juni 4, 2026 katika uwanja wa Mwabenda, Kata ya Solwa,
Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.
Kimandaguli FC iliingia uwanjani ikiwa na faida ya
ushindi wa mabao 3-1 walioupata katika mchezo wa kwanza, lakini Kashishi FC
walionesha dhamira ya kusaka ushindi na kufanikiwa kushinda mabao 2-0 ndani ya
dakika 90 za mchezo.
Matokeo hayo yaliifanya jumla ya mabao katika michezo
yote miwili kuwa sare ya 3-3, hali iliyolazimu mshindi kupatikana kwa mikwaju
ya penati kwa mujibu wa kanuni za mashindano hayo.
Katika hatua hiyo ya penati, Kimandaguli FC walionesha
utulivu na umakini mkubwa kwa kufanikiwa kushinda kwa penati 6-5 na hivyo
kuendelea na safari yao ya kuwania ubingwa wa NIACHEKONA CUP 2026, huku
Kashishi FC wakihitimisha safari yao katika mashindano hayo.
Akizungumza baada ya mchezo huo, Katibu wa Kamati ya
Mashindano Sambayi Jilya ametangaza kuwa mchezo wa kesho utawakutanisha Mwakitolyo
No. 6 na Isenengeja FC katika pambano linalotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.
Ameendelea kuwakaribisha wananchi, wadau wa michezo na
mashabiki wa soka kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa Mwabenda ili kuendelea
kushuhudia vipaji vya vijana na burudani ya michezo inayotolewa kupitia
mashindano hayo.
Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na mdau
wa michezo Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA kwa ufadhili wa shirika
la Lushu Foundation, yakiwa na lengo la kuibua vipaji vya vijana, kuimarisha
amani na kukuza michezo katika jamii.
Kwa mawasiliano ya huduma za ushereheshaji wa shughuli
mbalimbali, matangazo na matukio ya kijamii, MC NIACHEKONA anapatikana kupitia
namba 0757 267 738.
Kikosi cha Kimandaguli FC na kocha wa timu.
Wachezaji wa Kimandaguli FC na Kashishi FC wakioneshana ushindani mkubwa katika mchezo wa marudiano katika ligi ya NIACHEKONA CUP 2026 uliochezwa katika uwanja wa Mwabenda.
Wachezaji wa Kimandaguli FC na Kashishi FC wakioneshana ushindani mkubwa katika mchezo wa marudiano katika ligi ya NIACHEKONA CUP 2026 uliochezwa katika uwanja wa Mwabenda.
Pambano kali likiendelea uwanjani huku timu zote zikisaka nafasi ya kutinga hatua inayofuata ya mashindano.
Wachezaji wa Kashishi FC wakishangilia moja ya mabao mawili yaliyowapeleka kwenye hatua ya mikwaju ya penalti.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254


























Post a Comment