" MC NIACHEKONA AVUNJA UKIMYA BAADA YA KUMALIZIKA NIACHEKONA CUP 2026

MC NIACHEKONA AVUNJA UKIMYA BAADA YA KUMALIZIKA NIACHEKONA CUP 2026

Mkurugenzi wa mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026, Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA, amewashukuru Watanzania, wadau wa michezo, washiriki na taasisi mbalimbali zilizochangia kufanikisha mashindano hayo yaliyomalizika salama baada ya zaidi ya mwezi mmoja wa ushindani.

Akizungumza mara baada ya fainali kumalizika katika Uwanja wa Mwabenda, Kata ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, MC NIACHEKONA amesema mashindano hayo yalianza rasmi Mei 16, 2026 yakishirikisha jumla ya timu 22 kutoka maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Shinyanga na mikoa jirani.

Amesema kati ya timu hizo, Kashishi FC kutoka Kata ya Solwa imefanikiwa kutwaa ubingwa wa mashindano hayo huku Ufukunyungu FC kutoka Mjini Shinyanga ikimaliza katika nafasi ya pili baada ya kufika fainali.

MC NIACHEKONA ametoa shukrani za dhati kwa wananchi na wadau wote waliojitokeza kuunga mkono mashindano hayo tangu mwanzo hadi mwisho.

"Nawashukuru Watanzania wote kwa kuweza kutusapoti. Nawashukuru Misalaba Media, Jambo FM, Lushu Foundation pamoja na wadau wengine wote tuliokuwa tukishirikiana nao katika kufanikisha mashindano haya," amesema.

Aidha, ametoa pongezi kwa Kamati ya Mashindano, waamuzi, watangazaji wa michezo na watu wote waliohusika katika usimamizi wa michuano hiyo, akisema mchango wao umewezesha mashindano hayo kumalizika kwa mafanikio makubwa na amani.

MC NIACHEKONA pia ameomba serikali kuendelea kuunga mkono juhudi za kuendeleza michezo ya vijana, akieleza kuwa mwitikio mkubwa wa wananchi na washiriki unaonesha umuhimu wa michezo katika jamii.

Amesema anaamini kupitia Ofisi ya Afisa Michezo wa Wilaya pamoja na mamlaka husika, ujumbe wake utafikishwa serikalini ili kuendelea kuweka mazingira mazuri ya maendeleo ya michezo na vipaji vya vijana.

Aidha, ameshukuru Serikali, Chama cha Mpira wa Miguu pamoja na taasisi mbalimbali za michezo ikiwemo SHIDEFA kwa ushirikiano na vibali vilivyowezesha mashindano hayo kufanyika kwa mujibu wa taratibu na sheria.

Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yalihusisha timu 22 ambazo ni Home Boys, Manheigana, Ufukunyungu FC, Mwasenge, Duara FC, Mwandutu, Shilima, Songambele Mhangu FC, Nyundo FC, Nzoza, Mahembe, Mawemiru FC, Nyandolwa FC, Bajaji FC, Shilabela FC, Lyabukande, Kimandaguli, Kashishi FC, Isenengeja, Mwakitolyo No. 6, Sangu FC na Bulige FC.

Mashindano hayo yameandaliwa na Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA kwa ufadhili wa Lushu Foundation, yakilenga kuibua vipaji vya vijana, kukuza michezo na kuimarisha mshikamano wa jamii.

KASHISHI FC YAANDIKA HISTORIA KWA KUTWAA UBINGWA WA NIACHEKONA CUP 2026

 SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post