" SHILABELA FC YATINGA HATUA YA TIMU 12 BORA BAADA YA KUIFUNGA LYABUKANDE 3-0, NIACHEKONA CUP 2026

SHILABELA FC YATINGA HATUA YA TIMU 12 BORA BAADA YA KUIFUNGA LYABUKANDE 3-0, NIACHEKONA CUP 2026

Na Mapuli Kitina Misalaba

Timu ya Shilabela FC imefanikiwa kutinga hatua inayofuata ya mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Lyabukande FC katika mchezo uliochezwa leo Juni 3, 2026 kwenye uwanja wa Mwabenda, Kata ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

Ikumbukwe kuwa katika mchezo wa kwanza kati ya timu hizo, Shilabela FC iliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Lyabukande FC. Hivyo, kwa matokeo ya leo ya mabao 3-0, Shilabela FC imefanikiwa kusonga mbele kwa jumla ya mabao 4-0 katika michezo yote miwili. Ushindi huo umeihakikishia Shilabela FC nafasi ya kutinga hatua ya timu 12 bora za mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026.

Kwa matokeo hayo, safari ya Lyabukande FC katika mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 imefikia tamati baada ya kushindwa kuhimili presha ya wapinzani wao Shilabela FC walioonesha kiwango kizuri mbele ya mashabiki waliojitokeza kwa wingi kushuhudia pambano hilo.

Akizungumza baada ya mchezo huo, Makamu Mwenyekiti wa mashindano ya NIACHEKONA CUP, Samwel Stephen, ametangaza kuwa mchezo unaofuata utachezwa kesho ambapo Kashishi FC itamenyana na Kimandaguli FC katika pambano linalotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.

Ameendelea kuwakaribisha wananchi, wadau wa michezo na mashabiki wa soka kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa Mwabenda ili kuendelea kushuhudia vipaji vya vijana na burudani ya michezo inayotolewa kupitia mashindano hayo.

Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na mdau wa michezo Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA kwa ufadhili wa shirika la Lushu Foundation, yakiwa na lengo la kuibua vipaji vya vijana, kuimarisha amani na kukuza michezo katika jamii.

Kwa mawasiliano ya huduma za ushereheshaji wa shughuli mbalimbali, matangazo na matukio ya kijamii, MC NIACHEKONA anapatikana kupitia namba 0757 267 738.


Post a Comment

Previous Post Next Post