" UVCCM YAWATAKA VIJANA KUHESHIMU MAMLAKA ZA UTEUZI

UVCCM YAWATAKA VIJANA KUHESHIMU MAMLAKA ZA UTEUZI





Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) umewataka vijana nchini kuwa na nidhamu, heshima kwa mamlaka za uteuzi, na kulinda misingi ya chama wanapotekeleza majukumu yao ya kikazi na kichama.


Wito huo ulitolewa na Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Mohammed Kawaida, alipozungumza na waandishi wa habari Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma baada ya kuapishwa kwa Makamu wa Rais, Deogratius Ndejembi, huku akisema kuwa nafasi aliyopewa kiongozi huyo ni mfano thabiti unaoonyesha vijana wanapaswa kuwa tayari kutumikia taifa kwa uadilifu, bidhi, na kujituma wanapopewa dhamana.


Kawaida alisisitiza kuwa viongozi vijana wanapopata nafasi za kuaminika wanapaswa kufanya kazi kwa weledi huku wakiepuka kiburi na majivuno, na badala yake wazingatie sheria, kanuni, na taratibu zilizowekwa na chama katika kutekeleza majukumu yao.


Aidha, aliwakumbusha vijana kuheshimu viongozi wazee na viongozi wastaafu kutokana na mchango wao mkubwa walioutoa katika kujenga taifa, akisisitiza kuwa kizazi cha sasa kinapaswa kujifunza kutoka kwa waliowatangulia bila kupoteza heshima kwa misingi ya kulinda maslahi ya chama na taifa.

Post a Comment

Previous Post Next Post