" SERIKALI KWA KUSHIRIKIANA NA SHIRIKA LA NANCY FOUNDATION KUWAPATIA BIMA YA AFYA WATOTO WA MITAANI MANISPAA YA SHINYANGA.

SERIKALI KWA KUSHIRIKIANA NA SHIRIKA LA NANCY FOUNDATION KUWAPATIA BIMA YA AFYA WATOTO WA MITAANI MANISPAA YA SHINYANGA.

Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Serikali katika Halmashauri ya manispaa ya Shinyanga kwa kushirikiana na Shirika lisilo la kiserikali la Nancy Foundation, imeweka mipango ya kuwapatia bima ya afya CHF watoto wanaoishi mitaani ili iwasaidie kwenye upatikanaji wa huduma ya matibabu.

Hayo yamezungumzwa na Mkuu wa idara ya maendeleo ya jamii Manispaa ya Shinyanga Bwana John Tesha kwenye zoezi la kutambua na kuchukua taarifa za watoto wanaoishi mitaani linaloratibiwa na mashirika mawili ya Mkoa wa Shinyanga Nancy Foundation na Ubongo learing kwa kushirikiana na idara ya maendeleo na ustawi wa jamii ktk Manispaa ya Shinyanga.

Tesha amesema mchakato wa  kuwapatia bima ya afya CHF watoto wa mitaani unaendelea huku akiwaomba watoto hao kutoa ushirikiano kwa viongozi juu ya taarifa muhimu za familia na maisha yao.

“Niwaombe watoto mtupe ushirikiano mmoja baada ya mwingine aongee matatizo yake tuyajue tuone namna ya kuwasaidia, tunataka tuwapatie Bima ya afya ili ukiwa unaumwa uende Hospitali ukatibiwe kwa sababu tiba ni muhimu sana sasa hili tunalifanya kwa kushirikiana na wazazi wenu mtupe ushirikiano kuwajua wazazi wenu tuunganishe kaya A na kaya B tupate kaya za watu wasiobungua watu sita mpewe Bima ya afya nyie kazi yenu ibaki tu kusoma na kutafuta maisha”.amesema Mgeni rasmi Tesha

Katika zoezi hilo watoto wamepatiwa zawadi ya vifaa vya shule ikiwemo daftari na karamu huku mgeni rasmi Bwana John Tesha akilipongeza shirika la Nancy Foundation kwa ubinifu huo unaolenga kuwasaidia na kuwatoa watoto katika mazingira magumu mitaani.

Kwa upande wake afisa ustawi wa jamii Manispaa ya Shinyanga Bi. Maria Okama amesema zoezi la kukusanya watoto wa mitaani ni endelevu huku akieleza malengo yaliyokusudiwa.

“Tulifanikiwa kupata watoto 18 na leo tumeongeza watoto wamefika jumla 30 lakini pia hili zoezi ni endelevu lengo la kuwepo hapa ni kuhakikisha kwamba tunachukua taarifa muhimnu za watoto lakini pia kufahamu watoto hawa wanatoka katika maeneo gani ili  baada ya hapa tuweze kuondoka na hawa watoto kuelekea katika familia zao tutaenda kuongeza na wazazi na walezi lakini pia tumepanga wiki ijayo tuweze kukutana na wazazi wa watoto hawa ili tuweze kuwapa elimu ya malezi na makuzi ya watoto lakini pia tuweze kuwapa miongozo ya namna ya kuishi na watoto hawa”.Amesema afisa ustawi wa jamii Maria Okama

Aidha baada ya shughuli hiyo limefanyika zoezi la kuwarudisha watoto katika familia zao ambapo maafisa ustawi wa jamii Manispaa ya Shinyanga wamewasihi wazazi na walezi kuhakikisha watoto hao wanahudhuria shuleni.

Mkuu wa idara ya maendeleo ya jamii Manispaa ya Shinyanga Bwana John Tesha akizungumza kwenye zoezi hilo la uchukuaji taarifa kwa watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani.

Afisa ustawi wa jamii Manispaa ya Shinyanga Bi. Maria Okama akizungumza kwenye zoezi hilo la kuchukua kutambua na kuchukua taarifa za watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani.

Afisa ustawi wa jamii Manispaa ya Shinyanga Bi. Maria Okama akizungumza kwenye zoezi hilo la kuchukua kutambua na kuchukua taarifa za watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani.

Afisa ustawi wa jamii Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Bi. Ansila Materu akitoa elimu kwa watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani.







Zoezi la kuwapakulia watoto chakula likiendelea katika ukumbi wa Mazingira center Manispaa ya Shinyanga.

Zoezi la kuwapakulia watoto chakula likiendelea katika ukumbi wa Mazingira center Manispaa ya Shinyanga.

Post a Comment

Previous Post Next Post