" BASHE ACHUKUA FOMU YA UBUNGE NZEGA MJINI, AWAOMBA WANANCHI KUSUBIRI UTARATIBU WA CHAMA

BASHE ACHUKUA FOMU YA UBUNGE NZEGA MJINI, AWAOMBA WANANCHI KUSUBIRI UTARATIBU WA CHAMA



Na Mwandishi wetu, Misalaba Media

Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Nzega Mjini, Hussein Mohamed Bashe, amechukua fomu ya kuwania tena nafasi ya ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), akieleza dhamira yake ya kuendelea kulitumikia jimbo hilo endapo atapewa ridhaa tena.

Akizungumza baada ya kuchukua fomu, Bashe amewaomba wananchi waendelee kuwa watulivu na kusubiri utaratibu wa ndani ya chama, huku akisisitiza kuwa iwapo jina lake litapitishwa, ataendelea kusukuma gurudumu la maendeleo katika jimbo hilo.

"Niwaombe wananchi wa Nzega Mjini waendelee kuwa wavumilivu wakati chama kikiendelea na mchakato wake wa ndani. Tukiendelea kushikamana, tutaendelea kusukuma mbele gurudumu la maendeleo kama tulivyofanya miaka yote," amesema Bashe.




🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

Post a Comment

Previous Post Next Post