" ITIKAFU YA KIISLAMU: MATUMIZI YA IBADA KATIKA KUSAKA SULUHISHO LA KITAIFA NA AMANI

ITIKAFU YA KIISLAMU: MATUMIZI YA IBADA KATIKA KUSAKA SULUHISHO LA KITAIFA NA AMANI

Tamko la Viongozi wa Taasisi za Kiislamu limeonesha namna ya kipekee ambavyo ibada na dini zinaweza kutumika kama suluhisho la changamoto za kitaifa. 

Viongozi hao waliamua kuingia kwenye Itikafu, ibada maalumu ya kujitenga na mengine yote ndani ya Msikiti, ili kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu, si tu kutoa dua, bali pia kutafakari njia sahihi ya kuivusha nchi.
Kama ilivyoelezwa katika tamko, Itikafu ilifanywa kufuata amri za Mungu za "Kimbilieni kwa Mola wenu" (Surat Addhaariyaat aya 50) na kutafuta ngazi ya kufikisha maombi kupitia ibada (Surah Al-Māʾidah: 35).
"Tumeona ni Muhimu kuwa na ibada hii ya itikafu baada ya matukio mazito yaliyoikumba nchi yetu siku ya uchaguzi mkuu..."
Hatua hii ya kiroho imesababisha maazimio thabiti yaliyolenga kurejesha amani, haki, na utulivu. Hii inasisitiza kwamba taasisi za Kiislamu zinatumia imani yao kama nguvu ya uongozi katika kipindi kigumu, huku wakiwaombea waliofariki na waliopata hasara, na kumsihi Mwenyezi Mungu awape nguvu na busara ya kukikabili kipindi hiki bila mpasuko.
Tamko hilo limehitimishwa kwa kuagiza Waislamu wote katika maeneo yao ya ibada (misikiti, madrasa, n.k.) kuendelea kumuomba Mwenyezi Mungu arejeshe na kudumisha amani iliyotetereka, kuashiria umuhimu wa jukumu la kila muumini katika ulinzi wa amani ya taifa.
Hali hiyo inatokana na ukweli kuwa japokuwa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2025 zilifanyika kwa njia ya amani na utulivu,upigaji kura nao ulianza vizuri katika mikoa mingi ambapo wananchi walijitokeza  kupiga kura kwa amani, bila vurugu baadhi ya mikoa kulijitokeza fujo zilizolenga 
kuvuruga zoezi la kupiga na kuhesabu kura.   
Katika vurugu hizo nyumba na vituo vya mafuta vilichomwa, miundombinu ya umma iliharibiwa, biashara za watu binafsi zilivamiwa na kuchomwa moto, vituo vya polisi vilishambuliwa, ofisi kadhaa za Chama kimoja cha siasa zilichomwa moto, majengo ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa yalivamiwa na kuchomwa. Kubwa zaidi watu walijeruhiwa na kupoteza maisha, wakiwemo askari ambao walijitokeza kulinda mali na maisha ya raia. 
Taasisi za Kiislamu nchini Tanzania, pamoja na kulaani matukio haya na kusikitishwa sana na vifo vilivyotokea, upotevu wa mali za watu na 
uharibifu wa miundo mbinu uliotendeka na kuhuzunishwa na hali hiyo inahuzunishwa zaidi na kuwapo hadi sasa kwa makundi ambayo
yanatoa matamko ambayo kwa maudhui yake yanachochea na kuamsha hasira kwa namna ambayo yanahatarisha amani, utulivu, 
mshikamano na umoja wuliojengwa kwa miaka mingi tangu kuasisiwa kwa Taifa.

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
✉️ info@eastafricanspirits.com

1 Comments

  1. Kwa karibu mwaka mmoja, mume wangu aliniacha mimi na watoto wetu wawili. Aliacha kujali, akaacha kupiga simu, na akaondoka kabisa. Nilikuwa nimevunjika moyo, nimechanganyikiwa, na karibu kupoteza tumaini. Kisha siku moja, rafiki yangu aliniambia kuhusu Dkt. Dawn, mtu wa kiroho aliyepewa kipawa na ulimwengu ili kuwasaidia watu kurejesha upendo na amani.

    Mwanzoni, nilikuwa na shaka, lakini kitu kuhusu maneno yake kilinipa amani. Aliniambia haswa kilichokuwa kibaya na kwamba mtu alikuwa ametupa uchawi mkali kututenganisha. Aliandaa kazi maalum ya kiroho na uchawi wa kuungana tena kwa ajili yangu - na ndani ya siku chache, mume wangu alinipigia simu ghafla, akilia na kuomba msamaha.

    Tangu wakati huo, maisha yangu hayajawahi kuwa sawa. Ndoa yetu sasa ni tamu na yenye furaha zaidi duniani. Tunapendana zaidi kuliko hapo awali, na nyumba yetu imejaa vicheko na baraka.

    Lakini sio hivyo tu - Dkt. Dawn pia alisaidia kuondoa bahati mbaya na nishati hasi iliyozunguka familia yetu. Tangu wakati huo, kila kitu kimekuwa laini: amani nyumbani kwetu, maendeleo ya kifedha, afya njema, na furaha safi.

    Ninashukuru ulimwengu kila siku kwa kuniongoza kwa Dkt. Dawn. Kwa kweli ni mtu mwenye nguvu na mwanga wa kimungu. Ikiwa unapitia hali yoyote - huzuni, bahati mbaya, au kuchanganyikiwa - usikate tamaa. Mfikie na uache ulimwengu ufanye kazi kupitia yeye ili kubadilisha hadithi yako, kama vile alivyobadilisha yangu.

    Wasiliana naye kwenye WhatsApp: +2349046229159

    dawnacuna314@gmail.com

    ReplyDelete

Post a Comment

Previous Post Next Post