" DERBY YA WACHIMBAJI YAMALIZIKA NYANDOLWA YAONDOKA NA ALAMA TATU BAADA YA KUIFUNGA BAJAJI FC KATIKA LIGI YA NIACHEKONA

DERBY YA WACHIMBAJI YAMALIZIKA NYANDOLWA YAONDOKA NA ALAMA TATU BAADA YA KUIFUNGA BAJAJI FC KATIKA LIGI YA NIACHEKONA


Na Mapuli Kitina Misalaba


Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Shinyanga Said Mankiligo ameipongeza ligi ya NIACHEKONA CUP 2026 kwa kuendelea kutoa nafasi kwa vijana wenye umri wa chini ya miaka 20 kushiriki mashindano hayo huku akisema yanaendana na maelekezo na mwelekeo wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) katika kukuza vipaji vya vijana.

Akizungumza katika mashindano hayo yanayoendelea kwenye uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa, Mankiligo amesema amefurahishwa na namna waandaaji wa ligi hiyo walivyowapa nafasi kubwa vijana wadogo kuonesha uwezo wao ndani ya uwanja.

Amesema mashindano hayo yana mchango mkubwa katika kusaidia timu mbalimbali za Mkoa wa Shinyanga kupata nafasi ya kuona na kuchagua wachezaji wenye vipaji badala ya kutegemea wachezaji wa gharama kubwa wasiokidhi ushindani wa ligi mbalimbali.

Katika mchezo wa leo, timu ya NYANDOLWA imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya BAJAJI FC katika pambano lililojaa ushindani mkubwa kwenye derby hiyo ya wachimbaji wa madini iliyochezwa katika uwanja wa Mwabenda.

Baada ya mchezo huo, Katibu wa Kamati ya Mashindano Sambayi Jilya ametangaza matokeo ya mchezo wa leo pamoja na kusoma ratiba ya mechi ya kesho ambapo timu ya SHILABELA itamenyana na LYABUKANDE FC katika mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa ndani ya mashindano hayo.

Aidha amewakaribisha wananchi na wadau wa michezo kuendelea kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa Mwabenda kushuhudia michezo hiyo ambayo imeendelea kuwa jukwaa la kuibua vipaji vya vijana kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya Mkoa wa Shinyanga.

Ligi hiyo imeandaliwa na Bwana Paul Daud Augustino kupitia udhamini wa Lushu Foundation kwa lengo la kuibua vipaji vya vijana, kuimarisha mshikamano wa jamii pamoja na kukuza michezo katika Mkoa wa Shinyanga.

Mbali na kuwa mwandaaji wa mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026, Bwana Paul Daud Augustino ni mdau mkubwa wa michezo katika Wilaya ya Shinyanga. Kwa huduma za ushereheshaji wa shughuli mbalimbali, matangazo pamoja na burudani unaweza kuwasiliana naye kupitia namba 0757 267 738.

Timu ya BAJAJI FC


 SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post