" DUARA FC YATUMA SALAMU KWA TIMU ZINGINE BAADA YA KUFUZU (5 -2), MWANDUTU FC YAAGA NIACHEKONA CUP 2026

DUARA FC YATUMA SALAMU KWA TIMU ZINGINE BAADA YA KUFUZU (5 -2), MWANDUTU FC YAAGA NIACHEKONA CUP 2026

Na Mapuli Kitina Misalaba

Timu ya DUARA FC imefanikiwa kutinga hatua inayofuata ya mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 baada ya mpinzani wake MWANDUTU FC kushindwa kufikia idadi ya mabao yaliyohitajika katika mchezo wa marudiano uliochezwa kwenye uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

Katika mchezo wa leo Mei 29, 2026, timu hizo zimetoka sare ya mabao 2-2 katika pambano lililokuwa na ushindani mkubwa huku mashabiki wakishuhudia burudani ya hali ya juu ndani ya dakika 90 za mchezo.

Ikumbukwe kuwa katika mchezo wa kwanza wa hatua hiyo ya mtoano, MWANDUTU FC walifungwa mabao 3-0 dhidi ya DUARA FC hali iliyowalazimu kuhitaji ushindi mkubwa katika mchezo wa leo ili waweze kufuzu hatua inayofuata.

Kutokana na sare ya mabao 2-2 ya leo, DUARA FC imefanikiwa kusonga mbele kwa jumla ya mabao 5-2 kwa hesabu ya michezo yote miwili ya marudiano.

Baada ya mchezo huo, viongozi wa MWANDUTU FC wamemshukuru mwandaaji wa mashindano hayo Paul Daud Augustino kwa kuwapa nafasi ya kushiriki katika mashindano hayo huku wakiahidi kurejea kwa nguvu zaidi katika awamu zijazo za ligi hiyo.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa mashindano ya NIACHEKONA CUP Samwel Stephen ametangaza ratiba ya mchezo wa kesho ambapo SONGAMBELE MHANGU kutoka kata ya Salawe itamenyana na SHILIMA FC kutoka Mkoa wa Mwanza katika pambano linalotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.

Aidha amewahimiza wananchi pamoja na wadau wa michezo kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa Mwabenda kuendelea kushuhudia burudani ya soka pamoja na vipaji vya vijana vinavyoendelea kuibuliwa kupitia mashindano hayo.

Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na Paul Daud Augustino kupitia ufadhili wa shirika la Lushu Foundation kwa lengo la kuibua vipaji vya vijana, kukuza michezo pamoja na kuimarisha mshikamano wa jamii kupitia soka.

Kwa huduma za ushereheshaji wa shughuli mbalimbali, matangazo pamoja na burudani unaweza kuwasiliana na MC NIACHEKONA kupitia namba 0757 267 738.

Kikosi cha Duara FC.

 SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post