Na Mapuli Kitina Misalaba
Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yanayoendelea katika
uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
yameendelea kushika kasi ambapo timu ya ISENENGEJA imeibuka na ushindi wa bao
1-0 dhidi ya MWAKITOLYO No.6 katika mchezo uliokuwa na ushindani mkubwa.
Baada ya mchezo huo, Katibu wa Kamati ya Mashindano
Sambayi Jilya ametangaza ratiba ya mchezo wa kesho ambapo timu ya SANGU FC
itamenyana na BULIGE FC katika pambano linalotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa
ndani ya ligi hiyo.
Aidha Sambayi ameendelea kuwahimiza wananchi wa jimbo
la Solwa pamoja na maeneo jirani kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa Mwabenda
kushuhudia michezo hiyo ambayo imeendelea kuwa jukwaa la kuibua vipaji vya
vijana kupitia soka.
Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na
Bwana Paul Daud Augustino kupitia ufadhili wa Lushu Foundation kwa lengo la
kuibua vipaji vya vijana, kukuza michezo pamoja na kuimarisha mshikamano wa
jamii kupitia soka.
Kwa huduma za ushereheshaji wa shughuli mbalimbali, matangazo pamoja na burudani wasiliana na MC NIACHEKONA kupitia namba 0757 267 738.
ISENENGEJA FC
Wachezaji wa ISENENGEJA na MWAKITOLYO No.6 wakioneshana ushindani mkubwa katika ligi ya NIACHEKONA CUP 2026 inayoendelea kwenye uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa.
Wachezaji wa ISENENGEJA na MWAKITOLYO No.6 wakioneshana ushindani mkubwa katika ligi ya NIACHEKONA CUP 2026 inayoendelea kwenye uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa.
Viongozi pamoja na wadau wa michezo wakifuatilia mchezo kati ya ISENENGEJA na MWAKITOLYO No.6.
Watangazaji wa mechi.
Mashabiki wakifuatilia mchezo wa ISENENGEJA dhidi ya MWAKITOLYO No.6 katika uwanja wa Mwabenda leo Mei 25, 2026.
Mashabiki wakifuatilia mchezo wa ISENENGEJA dhidi ya MWAKITOLYO No.6 katika uwanja wa Mwabenda leo Mei 25, 2026.
Mashabiki wakifuatilia mchezo wa ISENENGEJA dhidi ya MWAKITOLYO No.6 katika uwanja wa Mwabenda leo Mei 25, 2026.
Mashabiki wakifuatilia mchezo wa ISENENGEJA dhidi ya MWAKITOLYO No.6 katika uwanja wa Mwabenda leo Mei 25, 2026.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254









Post a Comment